WATOTO 17 WAFICHWA NA KUPATIWA MAFUNZO YA KIISLAM KWA SIRI

Watoto wa Kiislam
Hali ya taharuki imetanda katika mikoa ya Kilimanjaro na Arusha baada ya kugundulika mahali walipofichwa watoto 17 wakiwamo watatu wa familia moja wanaodaiwa kupotea tangu mwezi Februari mwaka jana  kwa madai ya kufundishwa  maadili ya imani ya dini ya kiislamu. 
Umati mkubwa wa wakazi wa mji wa Moshi wamejitokeza katika kata ya Pasua mjini Moshi  kushuhudia tukio la watoto hao wenye umri wa  kuanzia miaka miwili hadi 13 ambao walikuwa wanaishi kwa Bw.Abdelnasir Abrahamani ambaye ni mfanyabiashara wa nguo nchini Kenya. 
Akizungumza katika eneo la tukio mkuu wa wilaya ya Moshi Bw.Novatus Makunga amesema tatizo hilo kwa mji wa Moshi ni kubwa na kwamba kwa sasa nyumba hiyo imefungwa na kuondolewa watoto hao ili warejeshwe kwa wazazi hao wakati hatua za kisheria zikiendelea. 
Mmoja wa wazazi mwenye watoto watatu waliopotea tangu mwezi February mwaka jana na kukutwa katika nyumba hiyo Bw.Ramadhani Mohamedi amesema aligundua tukio hilo baada ya kukutana na mtoto wake wa kike barabarani na kumweleza mateso wanayoyapata huko.
Naye mfanyabiashara huyo Bw.Abdulinasir Abrahamani amesema nyumba hiyo ni familia na ndugu zao wa kiislamu lakini siyo kituo cha yatima, ila ni sehemu ya kutolea mafundisho ya dini ya kiislamu.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
  • AN AFRICAN MAN SOLVES A 270 YEARS OLD MATH PROBLEM
    AN AFRICAN MAN SOLVES A 270 YEARS OLD MATH PROBLEM Ibrahima Sambégou Diallo may have become the…
  • NATIONAL BANK OF COMMERCE VACANCIES - 2015
    NATIONAL BANK OF COMMERCE VACANCIES - 2015 This is your chance to belong to a world-class…
  • WE WON WITH POORLY EDUCATED - DONALD TRUMP
    Donald Trump sweeps to victory in Nevada Republican caucuses on Tuesday, finished more than 20 points…
  • GOODLUCK JONATHAN TO RECONCILE IN ZANZIBAR POLL STALEMATE
    Zanzibar. The Commonwealth has appointed former President Goodluck Jonathan to lead the charge for the…
  • ARUMERU: WANANCHI WAVAMIA SHAMBA LA MWEKEZAJI LA KARATU ESTATE
    WANANCHI WAVAMIA SHAMBA LA MWEKEZAJI Yafuatayo ni baaadhi ya mabango yaliyokutwa katika Karamu Estate…
  • UFAFANUZI KUHUSU BASTOLA NA RISASI ZA GWAJIMA
    BASTOLA NA RISASI ZA GWAJIMA Tarehe 30/03/2015 waandishi wa habari walifika kituo Kikuu cha Polisi…
  • * PAPA AOMBA MSAMAHA KWA KASHFA ZA KANISA KATOLIKI
    Vatican. Baba Mtakatifu Papa Francis ameomba radhi wakati anaongoza mkutano wa wiki tatu wa baraza la…
  • HAVE YOU READ TODAY UK FRONT PAGES NEWSPAPER? READ NOW
    HabaruDuniani brings to you UK front pages Newspaper at your finger tips. Please do not forget to like our…
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2014 - TANZANIA CSEE 2014 RESULT
    MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2014 BOFY HAPA CSEE 2014 RESULT CLICK HERE
  • MUHAMMAD ALI IS TEAM PACQUIAO
    Pacquiao and Muhammad Ali "My dad is Team Pacquiao all the way!" Everybody and their dog has…

SOCIALIZE

twitterfacebookgoogle plusemail

IN CASE YOU MISSED IT

FOR INSURANCE SERVICES CLICK HERE