Showing posts with label Kilimanjaro. Show all posts
Showing posts with label Kilimanjaro. Show all posts

Baadhi ya Watoto 18
Taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Geofrey Kamwela imeeleza kuwa hayo yalibainika katika mahojiano baina ya watoto na askari wa dawati la jinsia.
Alisema watoto hao wanatoka mikoa mbalimbali ikiwamo Tanga, Mara, Kagera, Mbeya na Dodoma.
Kamanda Kamwela alisema pia wamegundua kuwa watoto walikuwa wakiishi kwenye mazingira magumu ikiwamo kulala chini katika chumba kidogo.
Alisema polisi linawashikilia watu wawili (mume na mke) ambao wanatuhumiwa kuwahifadhi watoto hao.
Kamanda huyo alisema watoto hao wana umri wa kwenda shule, lakini walikuwa hawasomi.
Alisema polisi wanachunguza aina ya masomo ya dini waliyokuwa wakifundishwa.
“Lazima tuchunguze uhalali wa masomo ya dini waliyokuwa wakisoma ili tujue kama kweli watoto hawa walipelekwa na wazazi wao au la, kwa kuwa watoto hao walipaswa kuwa shuleni” alisema Kamanda Kamwela.
Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Novatus Makunga alisema watoto hao walikuwa wakiishi kwenye mazingira magumu, huku wakipewa adhabu kali ikiwamo kubeba matofali mgongoni pindi wanapokosea.
“Maelezo ya watoto yanaonyesha walikuwa wakiteswa, adhabu hizi kwa watoto ni kubwa, bado tunawachunguza ili tujue kila kitu na walichukuliwaje huko majumbani kwao,” alisema Makunga.
Alisema kwa wazazi watakaowatambua watoto wao, wanapaswa kwenda na uthibitisho ikiwamo cheti cha kuzaliwa au uthibitisho mwingine utakaoonyesha ni mzazi halisi.


WATOTO 17 WAFICHWA NA KUPATIWA MAFUNZO YA KIISLAM KWA SIRI

Watoto wa Kiislam
Hali ya taharuki imetanda katika mikoa ya Kilimanjaro na Arusha baada ya kugundulika mahali walipofichwa watoto 17 wakiwamo watatu wa familia moja wanaodaiwa kupotea tangu mwezi Februari mwaka jana  kwa madai ya kufundishwa  maadili ya imani ya dini ya kiislamu. 
Umati mkubwa wa wakazi wa mji wa Moshi wamejitokeza katika kata ya Pasua mjini Moshi  kushuhudia tukio la watoto hao wenye umri wa  kuanzia miaka miwili hadi 13 ambao walikuwa wanaishi kwa Bw.Abdelnasir Abrahamani ambaye ni mfanyabiashara wa nguo nchini Kenya. 
Akizungumza katika eneo la tukio mkuu wa wilaya ya Moshi Bw.Novatus Makunga amesema tatizo hilo kwa mji wa Moshi ni kubwa na kwamba kwa sasa nyumba hiyo imefungwa na kuondolewa watoto hao ili warejeshwe kwa wazazi hao wakati hatua za kisheria zikiendelea. 
Mmoja wa wazazi mwenye watoto watatu waliopotea tangu mwezi February mwaka jana na kukutwa katika nyumba hiyo Bw.Ramadhani Mohamedi amesema aligundua tukio hilo baada ya kukutana na mtoto wake wa kike barabarani na kumweleza mateso wanayoyapata huko.
Naye mfanyabiashara huyo Bw.Abdulinasir Abrahamani amesema nyumba hiyo ni familia na ndugu zao wa kiislamu lakini siyo kituo cha yatima, ila ni sehemu ya kutolea mafundisho ya dini ya kiislamu.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

SOCIALIZE

twitterfacebookgoogle plusemail

IN CASE YOU MISSED IT

FOR INSURANCE SERVICES CLICK HERE