Baadhi ya Watoto 18
Taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Geofrey Kamwela imeeleza kuwa hayo yalibainika katika mahojiano baina ya watoto na askari wa dawati la jinsia.
Alisema watoto hao wanatoka mikoa mbalimbali ikiwamo Tanga, Mara, Kagera, Mbeya na Dodoma.
Kamanda Kamwela alisema pia wamegundua kuwa watoto walikuwa wakiishi kwenye mazingira magumu ikiwamo kulala chini katika chumba kidogo.
Alisema polisi linawashikilia watu wawili (mume na mke) ambao wanatuhumiwa kuwahifadhi watoto hao.
Kamanda huyo alisema watoto hao wana umri wa kwenda shule, lakini walikuwa hawasomi.
Alisema polisi wanachunguza aina ya masomo ya dini waliyokuwa wakifundishwa.
“Lazima tuchunguze uhalali wa masomo ya dini waliyokuwa wakisoma ili tujue kama kweli watoto hawa walipelekwa na wazazi wao au la, kwa kuwa watoto hao walipaswa kuwa shuleni” alisema Kamanda Kamwela.
Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Novatus Makunga alisema watoto hao walikuwa wakiishi kwenye mazingira magumu, huku wakipewa adhabu kali ikiwamo kubeba matofali mgongoni pindi wanapokosea.
“Maelezo ya watoto yanaonyesha walikuwa wakiteswa, adhabu hizi kwa watoto ni kubwa, bado tunawachunguza ili tujue kila kitu na walichukuliwaje huko majumbani kwao,” alisema Makunga.
Alisema kwa wazazi watakaowatambua watoto wao, wanapaswa kwenda na uthibitisho ikiwamo cheti cha kuzaliwa au uthibitisho mwingine utakaoonyesha ni mzazi halisi.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
  • MAWAZIRI WAWILI WAHUKUMIWA KWENDA JELA, KATIBU MKUU AACHIWA HURU
    Jamhuri ya Muungano wa Tanzania dhidi ya: Basili Mramba Daniel Yona Gray Mgonja Mahakama ya hakimu…
  • Wananchi wa Mwanza Wabomoa ujenzi wa Mtaa wa Makoroboi
    Wananchi wakiboboa Nguzo katika mtaa wa Makoroboi, Mwanza Normal 0 false false …
  • 13 NEW FACES IN RC RESHUFFLE
    President of Tanzania John Magufuli released the long awaited line-up of regional commissioners (RCs) that…
  • MAGAZETI YA LEO
    Kama kawaida Habari Duniani inakupa vichwa vya habari vya magazeti yote ya kila siku. Leo pia…
  • KURA YA MAONI YA KATIBA INAYOPENDEKEZWA YAHAIRISHWA
    KURA YA MAONI YA KATIBA YAHAIRISHWA Tume ya Taifa ya uchaguzi (NEC) imesema kuwa kura ya maoni ya…
  • HONGERA JAKAYA KIKWETE KWA KUTIMIZA MIAKA 65
    Tarehe kama ya Leo miaka 65 iliyopita Raisi wa awamu ya nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndugu,…
  • $ 92 ML CREDIT FROM INDIA TO IMPROVE WATER ACCESSIBILITY IN ZANZIBAR
    Dar es Salaam, Tanzania. Indian Prime Minister Narendra Modi and Tanzanian …
  • NESI AMCHAPA VIBOKO MJAMZITO NA MTOTO AFIA TUMBONI
    MANESI WAKISHIRIKISHANA JAMBO Muuguzi aliyekuwa zamu katika kituo cha Afya cha Muungano wilayani…
  • 3 WAYS TO AVOID WHATSAPP FEE OR TRIAL PERIOD
    Are you the power user of WhatsApp? Before getting started, let me clear that we all know and use…
  • ACACIA TAX FEUD: EXECUTIVE CHAIRMAN MET WITH TANZANIA PRESIDENT
    Tanzania’s President met with Barrick Gold Corp. Executive Chairman John Thornton in an effort to…

SOCIALIZE

twitterfacebookgoogle plusemail

IN CASE YOU MISSED IT

FOR INSURANCE SERVICES CLICK HERE