Magu, Mwanza watu wanaodhaniwa kuwa majambazi wakiwa na silaha za moto usiku wa kuamkia jana walifunga Mtaa wa Kisesa Kata ya Kisesa, Wilaya ya Magu mkoani Mwanza na kumuua mfanyabiashara Nestory Andrew umbali wa mita 50 kilipo Kituo cha Polisi.
Tukio hilo lilitokea saa 8:00 usiku, majambazi hayo yalifunga Barabara ya Mwanza-Musoma kwa muda na kusababisha taharuki kwa wakazi wa Kisesa huku milio ya bunduki ikitawala anga.
Wakizungumza na Habari Duniani eneo la tukio jana, mashuhuda walisema walianza kusikia milio mizito ya vitu kama bomu na kwamba baada ya muda wakaona watu wakivamia duka la mfanyabiashara huyo na kupiga risasi hewani.
Mmoja ya mashuhuda hao, alisema “Mimi ni fundi baiskeli hapa stendi jana (juzi) muda kama wa saa mbili usiku nilisikia sauti ya vishindo kama bomu, lakini baada ya muda nikasikia sauti za bunduki hewani,”

Aliongeza: “Kwa kweli tulitawanyika watu wote hapa mtaani na kuacha mali zetu. Baada ya kutulia tulikuja kushuhudia nini kilitokea, lakini tulikuta mtu mmoja ambaye ni mfanyabiashara hapa Kisesa anavuja damu tulimuangalia tukamkuta amefariki.”
Shuhuda mwingine, alisema watu hao walifunga Barabara ya Mwanza-Musoma na kwamba, walikuwa wakipiga risasi ovyo hewani.

Aliendelea kusema hali ilikuwa mbaya, kwani hawakuwahi kushuhudia tukio kama hilo na mtu aliyefariki alikuwa mfanyabiashara maarufu Kisesa.
Mwandishi wa habari hizi jana alifika Kituo cha Polisi Kisesa ambako askari wa kituo hicho walikiri kuwapo kwa tukio hilo huku wakitaka atafutwe Kamanda wa Polisi wa Wilaya ya Magu.

Kamanda wa Polisi Magu, Charles Mkapa alithibitisha kutokea kwa tukio hilo, lakini akadai msemaji mkuu ni Kamanda wa Polisi Mwanza.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Robert Mnyandwa alimtaja mfanyabiashara aliyefariki baada ya kupigwa risasi na majambazi hao kuwa ni Nestory Andrew mkazi wa Igoma.

Mnyandwa alisema hivi sasa wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo na kwamba, hata thamani ya mali na fedha zilizoporwa haijajulikana kwani mhusika alifariki dunia.
“Ni kweli tukio limetokea jana saa mbili usiku na mtu mmoja ambaye ni mfanyabiashara wa Kisesa alipigwa risasi na kupoteza maisha. Bado hatujamkamata mtu na tunaendelea na uchunguzi,” alisema Mnyandwa.

Kufungwa kwa mitaa na majambazi, kumesababisha wafanyabiashara hasa wanaojihusisha na biashara ya fedha kwa mitandao kufunga maduka yao mapema.
Wafanyabiashara kadhaa wamekwishauawa ama kuporwa fedha zao kutokana na majambazi hayo kuvamia maduka yao.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
  • WHATSAPP, iMESSAGE AND SNAPCHAT COULD BE BANNED
    WhatsApp iMessage Snapchat …
  • MAGUFULI SACK TANZANIA ANTI-CORRUPTION BODY CHIEF DR.HOSEAH
    Tanzania President Dr. Magufuli sacks Director General of The Prevention and Combating of Corruption…
  • * WABUNGE WAPYA WA UKAWA (CUF, CHADEMA, NLD NA NCCR-MAGEUZI)
    MAJIMBO MAPYA YA UKAWA (CUF, CHADEMA, NLD NA NCCR-MAGEUZI) James Mbatia ashinda Ubunge…
  • ACT - TANZANIA vs ACT-WAZALENDO
    ACT-TANZANIA ACT-TANZANIA DHIDI YA ACT-WAZALENDO ACT-WAZALENDO Zitto alijiunga…
  • 5 BORA YA CCM URAISI 2015
    CCM imeyatangaza majina matano yaliyopitishwa na Kamati ya CCM (CC) MAJINA MATANO 1. Bernard Membe 2.…
  • 2ND MINERAL SANDS REPORT:LIST OF MANY TO BE INTERROGATED
    Dar es Salaaam. Speaking at the State House yesterday after receiving a report from an eight-member team led…
  • 36 SPECIAL SEATS MP'S FOR CHADEMA, 10 FOR CUF AND 64 FOR CCM
    October 25, 2015 Tanzania voted for General Elections which resulted to increase in number of special seats…
  • MAJIMBO MAPYA 26 YA UCHAGUZI
    TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI MAJIMBO MAPYA 26 YA UCHAGUZI BAADA YA KUGAWANYWA
  • 3,000 Pupils share single Latrine, 250 make 1 Class.
    Teacher delivers a lesson GEITA. Students and staff at Ukombozi and Nyankumbu primary schools in Geita…
  • THIERRY HENRY WOMAN LOOK IN WALES
    THIERRY HENRY THIERRY HENRY AVAA WIGI Aliyekuwa mshambulizi mahiri aliyewai kuchezea timu ya Arsenal ya…

SOCIALIZE

twitterfacebookgoogle plusemail

IN CASE YOU MISSED IT

FOR INSURANCE SERVICES CLICK HERE