Baada ya kufungwa na Kenya, timu ya Tanzania imeibuka na kuifunga Nigeria kwa wiketi tatu katika mwendelezo wa michuano ya kufuzu kucheza kombe la Dunia kwa kwa wavulana chini ya miaka 19 inayoendelea Dar es Salaam.

Mechi hiyo ilifanyika Katika uwanja wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam huku Nigeria wakipata nafasi ya ku-tosi na kupata mikimbio 105
Wenyeji walifanikiwa kupata mikimbio 108 na kupoteza wiketi 7 katika zamu yao huku Salum Jumbe akipata mikimbio 45 katika mipira 64 aliyopiga. Kwa upande wa Nigeria, Akachukwu Chima alifanikiwa kupata mikimbio 22 katika mipira 50 aliyopiga.
Matumaini ya wenyeji Tanzania kufuzu yaliingia doa baada ya kufungwa kwa Kenya kwa runs 11 katika mechi nzuri ya kuvutia ya kufuzu iliyochezwa katika uwanja wa Gymkhana Dar es Salaam.

Hiyo ilikuwa ni mechi ya pili kwa wenyeji kupoteza, hivyo kutoa nafasi kwa Namibia, iliyoshinda mechi zote nne, baada ya kuwafunga Uganda kwa runs 39 katika mechi iliyofanyika Gymkhana Club.
Botswana pia iliwafunga Kenya kwa mikimbio 10 katika mechi iliyochezwa uwanja wa Annadil Burhani.
Michuano hiyo inaisha Alhamis na Namibia ikiwa na pointi 8 baada ya kushinda mechi zote, ikiwa katika nafasi nzuri ya kufuzu kucheza Kombe la Dunia, kutegemea na matokeo ya mechi za leo.

Wenyeji Tanzania , Kenya na Uganda (zote zikiwa na pointi 4 kila moja) pia zina nafasi ya kufuzu na kugombania nafasi ya pili ili kucheza katika michuano ya mwisho ya kufuzu itakayofanyika Bangladesh kwa ajili ya kutafuta tiketi ya mwisho, endapo Namibia itafuzu..
Nigeria na Botswana zina nafasi finyu baada ya kila moja kuwa na pointi 2 katika michezo mine iliyocheza (kila moja).
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
  • KETER - NATIONAL ASSEMBLY SPEAKER BLOCKS WAIGURU IMPEACHMENT MOTION
    Nandi Hills MP Alfred Keter Alfred Keter Nandi Hills MP has now accused National Assembly Speaker Justin…
  • 6 TOP OFFICIAL OF TANZANIA REVENUE SUSPENDED OVER 80 BILLION UNCOLLECTED TAX
    Tanzania Revenue Authority (TRA) Commissioner General Rished Bade suspended President John Magufuli has…
  • WAS OBAMA OR ZUMA RIGHT?
    During the 70th session of the United Nations General Assembly at United Nations headquarters in New York,…
  • .MZEE ALIYECHORA NEMBO YA TAIFA AFARIKI DUNIA
    Mzee Francis Maige Kanyasi alipolazwa Hospitali. Dar es Salaam, Muhimbili. Hospitali ya Taifa ya…
  • 36 SPECIAL SEATS MP'S FOR CHADEMA, 10 FOR CUF AND 64 FOR CCM
    October 25, 2015 Tanzania voted for General Elections which resulted to increase in number of special seats…
  • How will the Premier League Table be Decided if Two teams Finish Tied at the Top of the Table?
    The pair are not only level on points, but on goals scored, goals conceded, wins, draws and…
  • ARMY LAND CRUISER STOLEN
    Kenya; There is mystery surrounds the disappearance of a Kenya Army Land Cruiser from the Embakasi…
  • J. WOLPER ANASWA AKITOKA NDANI YA JUMBA LA FREEMASON DAR ES SALAAM
    Pichani msanii wa sinema za Kibongo Wolper Mshtuko! Staa wa sinema za Kibongo, Jacqueline Wolper Massawe…
  • WATOTO WA VIGOGO BOT WANAKESI YA KUJIBU NA TUHUMA ZA KUGHUSHI VYETI
    Benki Kuu ya Tanzania (BoT) WAFANYAKAZI wanane wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), wanaokabiliwa na tuhuma za…
  • * TANZANIA BANS THE USE OF PUBLIC FUNDS ON CHRISTMAS AND NEW YEAR CARDS
    The government of Tanzania yesterday banned printing and distributing festive season cards ahead of this…

SOCIALIZE

twitterfacebookgoogle plusemail

IN CASE YOU MISSED IT

FOR INSURANCE SERVICES CLICK HERE