Baada ya kufungwa na Kenya, timu ya Tanzania imeibuka na kuifunga Nigeria kwa wiketi tatu katika mwendelezo wa michuano ya kufuzu kucheza kombe la Dunia kwa kwa wavulana chini ya miaka 19 inayoendelea Dar es Salaam.

Mechi hiyo ilifanyika Katika uwanja wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam huku Nigeria wakipata nafasi ya ku-tosi na kupata mikimbio 105
Wenyeji walifanikiwa kupata mikimbio 108 na kupoteza wiketi 7 katika zamu yao huku Salum Jumbe akipata mikimbio 45 katika mipira 64 aliyopiga. Kwa upande wa Nigeria, Akachukwu Chima alifanikiwa kupata mikimbio 22 katika mipira 50 aliyopiga.
Matumaini ya wenyeji Tanzania kufuzu yaliingia doa baada ya kufungwa kwa Kenya kwa runs 11 katika mechi nzuri ya kuvutia ya kufuzu iliyochezwa katika uwanja wa Gymkhana Dar es Salaam.

Hiyo ilikuwa ni mechi ya pili kwa wenyeji kupoteza, hivyo kutoa nafasi kwa Namibia, iliyoshinda mechi zote nne, baada ya kuwafunga Uganda kwa runs 39 katika mechi iliyofanyika Gymkhana Club.
Botswana pia iliwafunga Kenya kwa mikimbio 10 katika mechi iliyochezwa uwanja wa Annadil Burhani.
Michuano hiyo inaisha Alhamis na Namibia ikiwa na pointi 8 baada ya kushinda mechi zote, ikiwa katika nafasi nzuri ya kufuzu kucheza Kombe la Dunia, kutegemea na matokeo ya mechi za leo.

Wenyeji Tanzania , Kenya na Uganda (zote zikiwa na pointi 4 kila moja) pia zina nafasi ya kufuzu na kugombania nafasi ya pili ili kucheza katika michuano ya mwisho ya kufuzu itakayofanyika Bangladesh kwa ajili ya kutafuta tiketi ya mwisho, endapo Namibia itafuzu..
Nigeria na Botswana zina nafasi finyu baada ya kila moja kuwa na pointi 2 katika michezo mine iliyocheza (kila moja).
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
  •   253 MAJIMBO UKAWA WAMEGAWANA, TABORA MJINI GUMZO NA MENGINE 11
      Majimbo hayo yalitangazwa na wawakilishi wa makatibu wakuu wa UKAWA, John Mnyika (Chadema),…
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2014 - TANZANIA CSEE 2014 RESULT
    MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2014 BOFY HAPA CSEE 2014 RESULT CLICK HERE
  • PROF.IBRAHIM LIPUMBA AJIONDOA CUF NA UKAWA
    LIPUMBA AJIONDOA UKAWA Prof. Ibrahim Lipumba, aliyekua mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF)…
  • TODAY NEWSPAPER FRONT PAGES - TANZANIA
    Today Tanzania newspapers HabariDuniani brings Tanzania newspaper headlines at your finger tips. THE…
  • ARUMERU: WANANCHI WAVAMIA SHAMBA LA MWEKEZAJI LA KARATU ESTATE
    WANANCHI WAVAMIA SHAMBA LA MWEKEZAJI Yafuatayo ni baaadhi ya mabango yaliyokutwa katika Karamu Estate…
  • GOOGLE SALUTES TANZANIA INDEPENDENCE DAY
    GOOGLE has saluted Tanzanians on the Independence celebration by removing one O and put the nation…
  • LOWASSA AKARIBISHWA UKAWA KUPITIA CHADEMA
    Lowassa ajiunga Chadema Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) umesema umemkaribisha rasmi Waziri Mkuu…
  • 10 FACTORS TO RAISE INSURANCE INDUSTRY IN TANZANIA
    How can Tanzania grow the sector and exploit the unique combination of factors Africa has in her…
  • How Cellphone can damage your sexual organs, pregnant women and Children?
    Are you keeping your phone in your pocket? …
  • Floyd Mayweather vs Manny Pacquiao
    Pambano la masumbwi linalosubiriwa na ulimwengu mzima kati ya mabondia wawili bora katika miaka ya hivi…

SOCIALIZE

twitterfacebookgoogle plusemail

IN CASE YOU MISSED IT

FOR INSURANCE SERVICES CLICK HERE