Baada ya kufungwa na Kenya, timu ya Tanzania imeibuka na kuifunga Nigeria kwa wiketi tatu katika mwendelezo wa michuano ya kufuzu kucheza kombe la Dunia kwa kwa wavulana chini ya miaka 19 inayoendelea Dar es Salaam.

Mechi hiyo ilifanyika Katika uwanja wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam huku Nigeria wakipata nafasi ya ku-tosi na kupata mikimbio 105
Wenyeji walifanikiwa kupata mikimbio 108 na kupoteza wiketi 7 katika zamu yao huku Salum Jumbe akipata mikimbio 45 katika mipira 64 aliyopiga. Kwa upande wa Nigeria, Akachukwu Chima alifanikiwa kupata mikimbio 22 katika mipira 50 aliyopiga.
Matumaini ya wenyeji Tanzania kufuzu yaliingia doa baada ya kufungwa kwa Kenya kwa runs 11 katika mechi nzuri ya kuvutia ya kufuzu iliyochezwa katika uwanja wa Gymkhana Dar es Salaam.

Hiyo ilikuwa ni mechi ya pili kwa wenyeji kupoteza, hivyo kutoa nafasi kwa Namibia, iliyoshinda mechi zote nne, baada ya kuwafunga Uganda kwa runs 39 katika mechi iliyofanyika Gymkhana Club.
Botswana pia iliwafunga Kenya kwa mikimbio 10 katika mechi iliyochezwa uwanja wa Annadil Burhani.
Michuano hiyo inaisha Alhamis na Namibia ikiwa na pointi 8 baada ya kushinda mechi zote, ikiwa katika nafasi nzuri ya kufuzu kucheza Kombe la Dunia, kutegemea na matokeo ya mechi za leo.

Wenyeji Tanzania , Kenya na Uganda (zote zikiwa na pointi 4 kila moja) pia zina nafasi ya kufuzu na kugombania nafasi ya pili ili kucheza katika michuano ya mwisho ya kufuzu itakayofanyika Bangladesh kwa ajili ya kutafuta tiketi ya mwisho, endapo Namibia itafuzu..
Nigeria na Botswana zina nafasi finyu baada ya kila moja kuwa na pointi 2 katika michezo mine iliyocheza (kila moja).
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
  • GERMANY COMMITS 175 MILLION USD FOR DEVELOPMENT IN TANZANIA
    German-Tanzania development cooperation over the next years will focus on strengthening Financial and…
  • 20 BOKO HARAM KILLED BY NIGER SOLDIERS
    At least 20 members of the Islamist militia Boko Haram group were killed on Wednesday in Southern Niger by…
  • What is the best vehicle manufactured in Afrika? One of them is luxury.
    Kiira EV- interior infront Kiira EV - UGANDA This is a car developed in Uganda by Kiira Motors…
  • IS YAMCHOMA MOTO RUBANI WA JORDAN HADI KUFA
    Serikali ya Jordan imesema itachukua hatua kali za kulipiza kisasi kufuatia kundi la IS kutoa…
  • AJALI YA TRENI NA LORI
    AJALI …
  • WALIOWAJERUHI POLISI TANZANIA TANGA WANASAKWA
    Polisi nchini Tanzania wamesema wanawasaka watuhumiwa waliowajeruhi askari sita kwa risasi mkoani…
  • PICTURE OF THE DAY.
    Our picture of the day 10/06/2016 is coming from France at the Stade de France. In Euro 2016, when…
  • 3 DAYS STATE VISIT TO ISRAEL - UHURU
    President Uhuru Kenyatta is seen off by Deputy President William Ruto President Uhuru Kenyatta left for…
  • Relationship between Arsenal and Manchester City
    Arsenal and Manchester City have had numerous connections over the past 30 years, especially with a…
  • AJIRA KWA WATANZANIA KATIKA SHIRIKA LA NDEGE LA EMIRATES KWA 2015
    UTANGULIZI Tarehe 22 Januari, 2015 kuanzia saa tano hadi sita mchana, Wizara inatarajia kuongea na…

SOCIALIZE

twitterfacebookgoogle plusemail

IN CASE YOU MISSED IT

FOR INSURANCE SERVICES CLICK HERE