Baada ya kufungwa na Kenya, timu ya Tanzania imeibuka na kuifunga Nigeria kwa wiketi tatu katika mwendelezo wa michuano ya kufuzu kucheza kombe la Dunia kwa kwa wavulana chini ya miaka 19 inayoendelea Dar es Salaam.

Mechi hiyo ilifanyika Katika uwanja wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam huku Nigeria wakipata nafasi ya ku-tosi na kupata mikimbio 105
Wenyeji walifanikiwa kupata mikimbio 108 na kupoteza wiketi 7 katika zamu yao huku Salum Jumbe akipata mikimbio 45 katika mipira 64 aliyopiga. Kwa upande wa Nigeria, Akachukwu Chima alifanikiwa kupata mikimbio 22 katika mipira 50 aliyopiga.
Matumaini ya wenyeji Tanzania kufuzu yaliingia doa baada ya kufungwa kwa Kenya kwa runs 11 katika mechi nzuri ya kuvutia ya kufuzu iliyochezwa katika uwanja wa Gymkhana Dar es Salaam.

Hiyo ilikuwa ni mechi ya pili kwa wenyeji kupoteza, hivyo kutoa nafasi kwa Namibia, iliyoshinda mechi zote nne, baada ya kuwafunga Uganda kwa runs 39 katika mechi iliyofanyika Gymkhana Club.
Botswana pia iliwafunga Kenya kwa mikimbio 10 katika mechi iliyochezwa uwanja wa Annadil Burhani.
Michuano hiyo inaisha Alhamis na Namibia ikiwa na pointi 8 baada ya kushinda mechi zote, ikiwa katika nafasi nzuri ya kufuzu kucheza Kombe la Dunia, kutegemea na matokeo ya mechi za leo.

Wenyeji Tanzania , Kenya na Uganda (zote zikiwa na pointi 4 kila moja) pia zina nafasi ya kufuzu na kugombania nafasi ya pili ili kucheza katika michuano ya mwisho ya kufuzu itakayofanyika Bangladesh kwa ajili ya kutafuta tiketi ya mwisho, endapo Namibia itafuzu..
Nigeria na Botswana zina nafasi finyu baada ya kila moja kuwa na pointi 2 katika michezo mine iliyocheza (kila moja).
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
  • KINGUNGE: LOWASSA ANAKUBALIKA. CCM IMEPOTEZA MWELEKEO
    Kingunge Ngombale Mwiru ‘ametoroka’ chama hicho kutokana na kile alichokieleza kimepoteza…
  • ZITTO KABWE AHAMIA ACT-TANZANIA
    ZITTO KABWE Siasa za Tanzania kwa hivi sasa zimechukua mkondo mpya baada ya aliyekuwa mbunge wa Kigoma…
  • IS YAMCHOMA MOTO RUBANI WA JORDAN HADI KUFA
    Serikali ya Jordan imesema itachukua hatua kali za kulipiza kisasi kufuatia kundi la IS kutoa…
  • JAMES LEMBELI AONDOKA CCM
    James Lembeli James Lembeli, Mbunge wa Kahama aliyemaliza muda wake amekataa kubadili msimamo wake wa…
  • . UK DONATES KSH 500M TO KENYA FOR FIGHT DROUGHT
    Nairobi, Kenya: Britain will donate more than Sh500 million to complement Kenya’s efforts towards mitigating…
  • WATU MAARUFU WALIO BET KWA MAYWEATHER KUSHINDA
    P DIDDY Floyd Mayweather ndie mtu aliyepata pesa nyingi baada ya pambano akifuatiwa na Manny Pacquiao,…
  • How will the Premier League Table be Decided if Two teams Finish Tied at the Top of the Table?
    The pair are not only level on points, but on goals scored, goals conceded, wins, draws and…
  • 6,000 VILLAGES WILL BE CONNECTED WITH ELECTRICITY IN TANZANIA
    6,000 villages will be connected with electricity through the Rural Energy Agency (REA) phase three, the…
  • BRELA: BEI MPYA ZA USAJILI WA KAMPUNI NA JINA LA BIASHARA
    BUSINESS REGISTRATIONS AND LICENSING AGENCY …
  • HAVE YOU READ TODAY UK FRONT PAGES NEWSPAPER? READ NOW
    HabaruDuniani brings to you UK front pages Newspaper at your finger tips. Please do not forget to like our…

SOCIALIZE

twitterfacebookgoogle plusemail

IN CASE YOU MISSED IT

FOR INSURANCE SERVICES CLICK HERE