Dangote kutengeneza Bandari Mtwara
Alhaji Dangote akisikiliza maelezo ya eneo husika

Mtwara

Wakazi wa kijiji cha Mgao, kata Naumbu katika halmashauri ya wilaya ya Mtwara, wametoa hekari 2,500 kwa mwekezaji wa kiwanda cha saruji cha Dangote, Alhaji Aliko Dangote ili ajenge bandari itakayotumika kusafirisha saruji kutoka kiwandani hapo kwenda maeneo mbalimbali ya ndani na nje ya nchi.

Mwenyekiti wa kijiji hicho, Abrahaman Shah alimweleza bilionea huyo namba moja Afrika kuwa, wakazi wa kijiji chake wameridhia kumpatia eneo kwa ajili ya ujenzi wa bandari na kwamba ni imani yao mradi huo utatekelezwa haraka iwezekanavyo.
dangote in tanzania
Mwenyekiti wa Kijiji cha Mgao, Abrahaman Shah akitoa maeleketo

“Sisi wakazi wa Mgao tumekupatia eneo la hekari 2,500 la nchi kavu na bahari ili ujenge bandari, pia tunawapatia ukazi wa kudumu katika kijiji chetu, wewe, balozi na balozi mdogo wa Nigeria hapa nchini, wote ninyi kuanzia sasa ni wakazi wa kijiji cha Mgao,” alisema Mwenyekiti huyo na kuongeza; “Kijiji chetu kina wakazi 2026, Alhaji Dangote atakuwa mkazi wa 2029, Balozi Isihaka Majabu atakuwa mkazi wa 2027 na balozi mdogo Salisu Umaru atakuwa mkazi wa 2028…hawa ni wakazi wenzetu wa kijiji cha Mgao,” alisema.

Picha za Dangote akiwa Mtwara


Alhaji Dangote akiwasili
Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Bi Halima Dendegu,
akiwa na mwakilishi wa Dangote, Esther Baruti
Msafara
Msafara
dangote in tanzania
Alhaji Dangote akizungumza na wahandishi wa habari
dangote in tanzania
Ndege iliyomleta ikiondoka
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

SOCIALIZE

twitterfacebookgoogle plusemail

IN CASE YOU MISSED IT

FOR INSURANCE SERVICES CLICK HERE