Dangote kutengeneza Bandari Mtwara
Alhaji Dangote akisikiliza maelezo ya eneo husika

Mtwara

Wakazi wa kijiji cha Mgao, kata Naumbu katika halmashauri ya wilaya ya Mtwara, wametoa hekari 2,500 kwa mwekezaji wa kiwanda cha saruji cha Dangote, Alhaji Aliko Dangote ili ajenge bandari itakayotumika kusafirisha saruji kutoka kiwandani hapo kwenda maeneo mbalimbali ya ndani na nje ya nchi.

Mwenyekiti wa kijiji hicho, Abrahaman Shah alimweleza bilionea huyo namba moja Afrika kuwa, wakazi wa kijiji chake wameridhia kumpatia eneo kwa ajili ya ujenzi wa bandari na kwamba ni imani yao mradi huo utatekelezwa haraka iwezekanavyo.
dangote in tanzania
Mwenyekiti wa Kijiji cha Mgao, Abrahaman Shah akitoa maeleketo

“Sisi wakazi wa Mgao tumekupatia eneo la hekari 2,500 la nchi kavu na bahari ili ujenge bandari, pia tunawapatia ukazi wa kudumu katika kijiji chetu, wewe, balozi na balozi mdogo wa Nigeria hapa nchini, wote ninyi kuanzia sasa ni wakazi wa kijiji cha Mgao,” alisema Mwenyekiti huyo na kuongeza; “Kijiji chetu kina wakazi 2026, Alhaji Dangote atakuwa mkazi wa 2029, Balozi Isihaka Majabu atakuwa mkazi wa 2027 na balozi mdogo Salisu Umaru atakuwa mkazi wa 2028…hawa ni wakazi wenzetu wa kijiji cha Mgao,” alisema.

Picha za Dangote akiwa Mtwara


Alhaji Dangote akiwasili
Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Bi Halima Dendegu,
akiwa na mwakilishi wa Dangote, Esther Baruti
Msafara
Msafara
dangote in tanzania
Alhaji Dangote akizungumza na wahandishi wa habari
dangote in tanzania
Ndege iliyomleta ikiondoka
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
  • TANZANIA PORTS AND REVENUE AUTHORITY ON INTER-BANK SETTLEMENT SYSTEM
    The Director of National Payment System at BoT, Mr Bernard Dadi, said the Central bank agreed to extend…
  • * OFFICIAL COMPLAINTS CONCERNING 2015 ELECTIONS FROM LOWASSA
    My fellow citizens! Today on 29 October 2015, through my co-candidate, Hon. Juma Duni Haji have filed…
  • WAZIRI MKUU:CHAMA CHOCHOTE KINAWEZA KUSHIKA DOLA
    Waziri Mkuu Mizengo Pinda UPINZANI KUCHUKUA DOLA Chama chochote cha siasa nchini kina nafasi ya kushika…
  • Maandamano ya Kigoma yampa Ujumbe huu Dk.Slaa wa CHADEMA
    Ujumbe wa Dk.Slaa kutoka Kigoma …
  • * PAPA AOMBA MSAMAHA KWA KASHFA ZA KANISA KATOLIKI
    Vatican. Baba Mtakatifu Papa Francis ameomba radhi wakati anaongoza mkutano wa wiki tatu wa baraza la…
  • MORSI JELA MIAKA 20 MISRI
    Raisi wa Zamani wa Misri, Mohammed Morsi Misri. Makahama nchini Misri imemhukumu aliyekuwa rais wa…
  • RAISI KIKWETE AMETEUA WABUNGE WAWILI WAPYA
    ALI HASSAN MWINYI, JAKAYA KIKWETE, BENJAMINI MKAPA Raisi Jakaya Mrisho Kikwete:Ameteua wabunge wawili (2)…
  • What is the best vehicle manufactured in Afrika? One of them is luxury.
    Kiira EV- interior infront Kiira EV - UGANDA This is a car developed in Uganda by Kiira Motors…
  • WATOTO WA VIGOGO BOT WANAKESI YA KUJIBU NA TUHUMA ZA KUGHUSHI VYETI
    Benki Kuu ya Tanzania (BoT) WAFANYAKAZI wanane wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), wanaokabiliwa na tuhuma za…
  • MADUDU RIPOTI YA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI
    RIPOTI ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), imeibua ufisadi mkubwa katika mamlaka za…

SOCIALIZE

twitterfacebookgoogle plusemail

IN CASE YOU MISSED IT

FOR INSURANCE SERVICES CLICK HERE