Mohammed Dewji

TAJIRI KIJANA KULIKO WOTE AFRIKA


Mohammed Dewji has seen his net worth rise considerably over the past year as his MeTL group, a conglomerate in 11 countries with interests in trade, FMCG and manufacturing, undergoes significant expansion.

Mfanyabiashara maarufu nchini na Mbunge wa Singida Mjini (CCM), Mohammed Dewji (pichani) kwa mara ya kwanza ameingia kwenye orodha ya mabilionea 29, akiwa tajiri kijana kuliko wote barani Afrika.

Jarida la Forbes la Marekani limemtaja Dewji (39), katika nafasi ya 24 ya matajiri wa Afrika akiwa na utajiri wa Dola 1.3 bilioni za Marekani (Sh2.34 trilioni) unaotokana na biashara mbalimbali anazozifanya kupitia kampuni yake ya Mohammed Enterprises (Metl Group).“Dewji alibadilisha biashara aliyoanzisha baba yake kutoka uuzaji bidhaa na kuwa na viwanda vya Metl,” inasema sehemu ya habari inayomuhusu bilionea huyo Mtanzania .
“Alinunua viwanda vya nguo na mafuta vilivyokuwa vinamilikiwa na Serikali kwa bei ndogo na kuvifanya viwe na faida zaidi kwa kutumia mtindo wa kisasa wa menejimenti,” inaongeza ripoti hiyo.

Metl ina viwanda vya kutengeneza nguo na bidhaa nyingine za matumizi ya binadamu vikiwamo vyakula, sabuni na vinywaji. Pia ina mapato yanayozidi Dola 1.4 milioni za Marekani (Sh2.5 trilioni) kwa mwaka.
Katika kampuni hiyo, ambayo imekuwa na ushindani dhidi ya kampuni kubwa nyingine kama Said Salim Bakhresa, Dewji anamiliki asilimia 75 ya hisa zote.
Kwa mujibu wa tovuti yake, Metl inaendesha shughuli za uagizaji na usafirishaji bidhaa kutoka na kwenda nje, uzalishaji unaohusisha nguo, vinywaji na vyakula, usagaji nafaka, nishati na petroli na utengenezaji baiskeli.
Pia inahusika na huduma za simu, fedha, kilimo na pia ina kitengo cha kontena kwenye Bandari ya Dar es Salaam.

Dewji anashika nafasi mbili juu zaidi ya kada maarufu wa CCM na aliyekuwa mbunge wa Jimbo la Igunga, Aziz Rostam (50) aliyewekwa nafasi ya mwisho.
Rostam amefungana nafasi ya 26 na mabilionea wa Nigeria, Abdulsamad Rabiu na Femi Otedola wenye utajiri wa Sh1.8 trilioni kila mmoja.
Orodha hiyo ya 29 bora inaoongozwa na bilionea wa Nigeria, Aliko Dangote akiwa na utajiri wa Dola 15.7 bilioni za Marekani (Sh28.2 trilioni), kiwango ambacho ni mara moja na nusu ya bajeti ya Serikali ya Tanzania ya mwaka 2014/15.


Forbes linamtaja Rostam kuwa na utajiri wenye thamani ya Dola 1 bilioni za Marekani (Sh1.8 trilioni), kiwango ambacho kimebaki pasi na mabadiliko kutoka orodha ya mwaka jana. Rostam anamiliki asilimia 35 ya hisa katika kampuni ya huduma za simu za mkononi ya Vodacom.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
  • UK NEWS PAPERS
    Habari Duniani Media Limited brings UK News Paper in your finger tips. Read Today Uk News Papers…
  • 3 MILLIONS CROWDS PROTEST AGAINST BRAZIL'S PRESIDENT
    Widespread Anger against Brazilian President Dilma Rousseff is mounting as hundreds of thousands of people…
  • KITUO CHA RADIO KILICHOTANGAZA MAPINDUZI YA BURUNDI CHACHOMWA MOTO
    Kituo cha Radio Burundi …
  • AKUTWA NA FUNZA ZAIDI YA MIA MOJA 100
    Normal 0 false false false EN-US X-NONE X-NONE …
  • LOCAL INSURANCE FIRMS CHALLENGED
    Wilson Ndesanjo (Left) and Jean Razafimandimbly (Right) The insurance landscape is bound to change, with…
  • LIPUMBA AMTEMBELEA JOSEPHAT GWAJIMA
    Prof.Lipumba akiwa na Josephat Gwajima LIPUMBA AMTEMBELEA ASKOFU DR. JOSEPHAT GWAJIMA Profesa Ibrahim…
  • WAZIRI ASHINDWA UCHAGUZI NA KUMSHAMBULIA MSIMAMIZI
    Dk Titus Kamani ashindwa uchaguzi Hali ilikuwa mbaya jimboni Busega ambako baada ya Dk Kamani na wafuasi…
  • HAVE YOU READ TODAY UK FRONT PAGES NEWSPAPER? READ NOW
    HabaruDuniani brings to you UK front pages Newspaper at your finger tips. Please do not forget to like our…
  • 1 DECEMBER 2015 WORLD AIDS DAY EXHIBITION CANCELLED IN TANZANIA
    President of United Republic of Tanzania Dr. John Magufuli cancelled the climax of HIV and AIDS…
  • UKAWA WAANZA SAFARI YA URAISI 2015 TANZANIA
    Tangu mwaka huu uanze zimekuwapo pilikapilika nyingi za kisiasa ndani ya vyama vya siasa na Jumanne…

SOCIALIZE

twitterfacebookgoogle plusemail

IN CASE YOU MISSED IT

FOR INSURANCE SERVICES CLICK HERE