Dar es Salaam. Jumuiya ya Wanataaluma wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Udasa) na ITV/ Radio One wamesaini makubaliano ya kuandaa midahalo ya wagombea wa urais kwenye Uchaguzi Mkuu Oktoba mwaka huu.
Akizungumza baada ya kutia saini makubaliano hayo jana Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Udasa, Profesa Kitila Mkumbo alisema katika nchi za kidemokrasia midahalo hufanikisha uchaguzi ulio huru, haki na wazi.
Pia, alisema midahalo hiyo hutoa fursa muhimu kwa wagombea kueleza falsafa, sera na mikakati yao ya kutatua matatizo mbalimbali yanayowakabili wananchi.
Hata hivyo, Profesa Mkumbo alisema midahalo watakayoendesha haitaegemea chama chochote na kwamba mgombea atakayekataa kushiriki hawamlazimishi.
“Hatutakuwa na uwezo wa kumlazimisha mgombea, nchi hii ina historia ya wagombea kukimbia midahalo,” alisema Profesa Mkumbo.
Alisema muda rasmi wa kuanza kwa midahalo hiyo utatangazwa baadaye, wananchi wajue kuwa kupitia matangazo hayo wapiga kura watajua weledi na umahiri wa wagombea na vyama vyao.
“Tafiti zinaonyesha kuwa midahalo ya wagombea urais ina nafasi ya kipekee katika kuwawezesha wapiga kura kuamua mgombea gani wamchague,” alisema.
Alisema kuwa vyama vyote vitakavyoshiriki katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu na ambavyo vitasimamisha wagombea wa urais vitaalikwa kushiriki katika midahalo hiyo.
Pia wagombea wote watakaojitokeza kugombea urais katika Uchaguzi Mkuu mwaka huu wataalikwa kushiriki mdahalo huo.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa ITV na Radio One, Joyce Mhavile alisema midahalo hiyo itaaminiwa na wananchi kwa sababu wanaoandaa hawagombei nafasi yoyote katika uchaguzi huo.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
  • WATOTO WALIOFICHWA WAZUNGUMZA.
    Baadhi ya Watoto 18 Taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Geofrey Kamwela…
  • MAGUFULI SACK TANZANIA ANTI-CORRUPTION BODY CHIEF DR.HOSEAH
    Tanzania President Dr. Magufuli sacks Director General of The Prevention and Combating of Corruption…
  • KCPE AND UACE EXAMS KICK OFF IN KENYA AND UGANDA
    Kenya. A total of 937,467 candidates are set to start the Kenya Certificate of Primary Education examination…
  • KITUO CHA RADIO KILICHOTANGAZA MAPINDUZI YA BURUNDI CHACHOMWA MOTO
    Kituo cha Radio Burundi …
  • NATIONAL BANK OF COMMERCE VACANCIES - 2015
    NATIONAL BANK OF COMMERCE VACANCIES - 2015 This is your chance to belong to a world-class…
  • FORMER KENYA JUDICIARY CHIEF REGISTRAR SKIPS COURT
    Kenya. Former Judiciary Chief Registrar,Gladys Shollei did not appear in court on Tuesday to take plea…
  • TANZANIA-ZAMBIA RAILWAY TO BE EXTENDED TO FOUR OTHER COUNTRIES.
    China has pledged to finance the Tanzania-Zambia Railways (Tazara) and extend it to four other…
  • _ POPE TO VISIT KENYA, UGANDA AND CENTRAL AFRICAN REPUBLIC IN NOVEMBER
    Kenyas Catholic looks forward to Pope Francis’ first visit from November 25 to 27. On Sunday they will begin…
  • MFANYIE HAYA MAMBO 10 MPENZI WAKO UONE
    Mapenzi …
  • AKUTWA NA FUNZA ZAIDI YA MIA MOJA 100
    Normal 0 false false false EN-US X-NONE X-NONE …

SOCIALIZE

twitterfacebookgoogle plusemail

IN CASE YOU MISSED IT

FOR INSURANCE SERVICES CLICK HERE