Dar es Salaam. Jumuiya ya Wanataaluma wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Udasa) na ITV/ Radio One wamesaini makubaliano ya kuandaa midahalo ya wagombea wa urais kwenye Uchaguzi Mkuu Oktoba mwaka huu.
Akizungumza baada ya kutia saini makubaliano hayo jana Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Udasa, Profesa Kitila Mkumbo alisema katika nchi za kidemokrasia midahalo hufanikisha uchaguzi ulio huru, haki na wazi.
Pia, alisema midahalo hiyo hutoa fursa muhimu kwa wagombea kueleza falsafa, sera na mikakati yao ya kutatua matatizo mbalimbali yanayowakabili wananchi.
Hata hivyo, Profesa Mkumbo alisema midahalo watakayoendesha haitaegemea chama chochote na kwamba mgombea atakayekataa kushiriki hawamlazimishi.
“Hatutakuwa na uwezo wa kumlazimisha mgombea, nchi hii ina historia ya wagombea kukimbia midahalo,” alisema Profesa Mkumbo.
Alisema muda rasmi wa kuanza kwa midahalo hiyo utatangazwa baadaye, wananchi wajue kuwa kupitia matangazo hayo wapiga kura watajua weledi na umahiri wa wagombea na vyama vyao.
“Tafiti zinaonyesha kuwa midahalo ya wagombea urais ina nafasi ya kipekee katika kuwawezesha wapiga kura kuamua mgombea gani wamchague,” alisema.
Alisema kuwa vyama vyote vitakavyoshiriki katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu na ambavyo vitasimamisha wagombea wa urais vitaalikwa kushiriki katika midahalo hiyo.
Pia wagombea wote watakaojitokeza kugombea urais katika Uchaguzi Mkuu mwaka huu wataalikwa kushiriki mdahalo huo.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa ITV na Radio One, Joyce Mhavile alisema midahalo hiyo itaaminiwa na wananchi kwa sababu wanaoandaa hawagombei nafasi yoyote katika uchaguzi huo.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
  • VITAMBULISHO VYA UZANZIBARI VYAZUA BALAA
    Zanzibar VITAMBULISHO VYA UZANZIBARI VYAZUA BALAA Vyama vya upinzani Zanzibar, vimeshauri Sheria ya…
  • TANZANIA YAFUZU KUCHEZA KOMBE LA DUNIA
    Baada ya kufungwa na Kenya, timu ya Tanzania imeibuka na kuifunga Nigeria kwa wiketi tatu katika mwendelezo…
  •  *TANZANIA'S HOME AFFAIRS MINISTER SUSPENDED FOR ALCOHOLISM
    President John Magufuli of Tanzania has revoked appointment of Home Affair Minister Charles Kitwanga for…
  • 110 MAJINA YA WABUNGE WANAWAKE WA VITI MAALUM
    MAJINA YA WABUNGE WA VITI MAALUM UGAWAJI WA VITI MAALUM KWA KILA CHAMA CHA SIASA UNAZINGATIA IBARA YA 7891)…
  • 300 EMPLOYMENT OPPORTUNITY AT TRA
    300 people in different job positions this year will be employed by the Tanzania Revenue Authority (TRA) to…
  • * TANZANIA BANS THE USE OF PUBLIC FUNDS ON CHRISTMAS AND NEW YEAR CARDS
    The government of Tanzania yesterday banned printing and distributing festive season cards ahead of this…
  • WATANGAZA NIA WALIOENDA KWA TB JOSHUA
    Mwaka 2015 ni mwaka wa uchaguzi nchini Tanzania. Kupitia wanachama  mbalimbali nchini kutangaza nia…
  • MRI EQUIPMENT REPAIRED AT MUHIMBILI AFTER MAGUFULI VISIT
    Muhimbili National Hospital (File Photo) Muhimbili National Hospital (MNH) has announced that…
  • UN-TANZANIA WAS AN EXEMPLARY IN MAKING EDUCATION AVAILABLE FOR ALL
    On Sunday, The UN chief made the remarks when launching the International Commission on Financing Global…
  • JOBS AT PPF
    APRIL - JOBS AT PPF Job Title:Operations Trainee  Report To:Zonal Manager  Duties and…

SOCIALIZE

twitterfacebookgoogle plusemail

IN CASE YOU MISSED IT

FOR INSURANCE SERVICES CLICK HERE