Papa
Vatican. Baba Mtakatifu Papa Francis ameomba radhi wakati anaongoza mkutano wa wiki tatu wa baraza la makardinali na maaskofu kujadili namna ya kupitia mafundisho ya kanisa hilo pamoja na kuhusu masuala ya familia.
Papa Francis ameuomba msamaha huo alipokuwa akiwahubiria maelfu ya watu waliokusanyika kwenye Uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Peter, mjini Vatican, katika utaratibu wake wa kila juma.

''Kabla ya kuanza kwa Katekesi, nataka kwa niaba ya Kanisa, kuomba msamaha kwa kashfa ambazo hivi karibuni zimeikumba Roma na Vatican. Naomba msamaha wenu,'' alisema Papa Francis.
Msamaha huo ameuomba katika kipindi ambacho Kanisa Katoliki limejikuta kwenye kashfa kadhaa, ikiwemo ile ya kujitokeza hadharani kwa Padri shoga anayepinga msimamo wa kanisa kuhusu mapenzi ya jinsia moja na kauli dhidi ya Meya wa Roma, aliyejiuzulu wiki iliyopita.

Hata hivyo, Papa hakutaja hasa aina ya kashfa anayoizungumzia wala kutoa mifano. Siku moja kabla ya kuanza kwa mkutano huo kuhusu masuala ya familia, padri wa Poland alitangaza hadharani kuwa yeye ni shoga, huku mpenzi wake akiwa pembeni yake. Padri huyo aliyefanya kazi yake Vatican kwa miaka 17, alifukuzwa kazi yake ya ukasisi.
Krzysztof Charamsa, Polish Priest gay.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
  • Why People Don't Buy Life Insurance?
    1. It's sold by insurance agents: Let's be honest, most people that sell insurance aren't looked at…
  • How to save your Eyesight from Screens (Computer, Cellphone, Laptop and Television) ?
    Screen is everywhere (Computer, Cellphone, Laptop and TV) Right now you are staring at a screen, ah ah a!…
  • JAMES LEMBELI AONDOKA CCM
    James Lembeli James Lembeli, Mbunge wa Kahama aliyemaliza muda wake amekataa kubadili msimamo wake wa…
  • BELGIUM ON HIGH TERRORISM ALERT
    Belgium is on high alert after a major anti-terror raid in which two suspected Islamist militants were…
  • MAALIM SEIF SHARIF HAMAD ACHUKUA FOMU YA KUGOMBEA URAISI ZANZIBAR
    Mgombea Urais wa Zanzibar wa UKAWA kupitia Chama cha Wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad akionyesha…
  • Tanzania launches Sustainable Energy for All SE4ALL
    Dar es Salaam, Tanzania launches Sustainable Energy for All (SE4ALL) today at Julius Nyerere International…
  • 15 PATIENTS WITH CHOLERA IN MWANZA AND 7 IN KIGOMA, TANZANIA
    Mwanza. Cholera outbreak in Mwanza Region has been contained tremendously with current statistics showing…
  • AN AFRICAN MAN SOLVES A 270 YEARS OLD MATH PROBLEM
    AN AFRICAN MAN SOLVES A 270 YEARS OLD MATH PROBLEM Ibrahima Sambégou Diallo may have become the…
  • 2017 ACSEE EXAMINATION RESULTS
    Matokeo ya Kidato cha Sita yametangazwa rasmi na Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA). MATOKEO YA KIDATO…
  • 20 BOKO HARAM KILLED BY NIGER SOLDIERS
    At least 20 members of the Islamist militia Boko Haram group were killed on Wednesday in Southern Niger by…

SOCIALIZE

twitterfacebookgoogle plusemail

IN CASE YOU MISSED IT

FOR INSURANCE SERVICES CLICK HERE