Papa
Vatican. Baba Mtakatifu Papa Francis ameomba radhi wakati anaongoza mkutano wa wiki tatu wa baraza la makardinali na maaskofu kujadili namna ya kupitia mafundisho ya kanisa hilo pamoja na kuhusu masuala ya familia.
Papa Francis ameuomba msamaha huo alipokuwa akiwahubiria maelfu ya watu waliokusanyika kwenye Uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Peter, mjini Vatican, katika utaratibu wake wa kila juma.

''Kabla ya kuanza kwa Katekesi, nataka kwa niaba ya Kanisa, kuomba msamaha kwa kashfa ambazo hivi karibuni zimeikumba Roma na Vatican. Naomba msamaha wenu,'' alisema Papa Francis.
Msamaha huo ameuomba katika kipindi ambacho Kanisa Katoliki limejikuta kwenye kashfa kadhaa, ikiwemo ile ya kujitokeza hadharani kwa Padri shoga anayepinga msimamo wa kanisa kuhusu mapenzi ya jinsia moja na kauli dhidi ya Meya wa Roma, aliyejiuzulu wiki iliyopita.

Hata hivyo, Papa hakutaja hasa aina ya kashfa anayoizungumzia wala kutoa mifano. Siku moja kabla ya kuanza kwa mkutano huo kuhusu masuala ya familia, padri wa Poland alitangaza hadharani kuwa yeye ni shoga, huku mpenzi wake akiwa pembeni yake. Padri huyo aliyefanya kazi yake Vatican kwa miaka 17, alifukuzwa kazi yake ya ukasisi.
Krzysztof Charamsa, Polish Priest gay.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
  • KETER - NATIONAL ASSEMBLY SPEAKER BLOCKS WAIGURU IMPEACHMENT MOTION
    Nandi Hills MP Alfred Keter Alfred Keter Nandi Hills MP has now accused National Assembly Speaker Justin…
  • 36 SPECIAL SEATS MP'S FOR CHADEMA, 10 FOR CUF AND 64 FOR CCM
    October 25, 2015 Tanzania voted for General Elections which resulted to increase in number of special seats…
  • Today News paper front pages
    Have you read today News paper front page?
  • HAKI ZAKO UWAPO MIKONONI MWA POLISI.
    UWAPO MIKONONI MWA POLISI FANYA HAYA   1. Askari akikuweka chini ya ulinzi muulize…
  • BELGIUM ON HIGH TERRORISM ALERT
    Belgium is on high alert after a major anti-terror raid in which two suspected Islamist militants were…
  • MAJIMBO MAPYA 26 YA UCHAGUZI
    TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI MAJIMBO MAPYA 26 YA UCHAGUZI BAADA YA KUGAWANYWA
  • Maandamano ya Kigoma yampa Ujumbe huu Dk.Slaa wa CHADEMA
    Ujumbe wa Dk.Slaa kutoka Kigoma …
  • .MZEE ALIYECHORA NEMBO YA TAIFA AFARIKI DUNIA
    Mzee Francis Maige Kanyasi alipolazwa Hospitali. Dar es Salaam, Muhimbili. Hospitali ya Taifa ya…
  • SHERIA YA MAKOSA YA MTANDAO YAANZA RASMI TANZANIA
    Waziri wa Mawasilaiano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa(Mb), akiongea na waandishi wa…
  • UKAWA: WAMTAMBULISHA MGOMBEA URAISI MWANZA
    Viongozi wa Umoja wa Katiba ya Wananchi UKAWA, wamepokelewa kwa kishindo jijini Mwanza ikielezwa kuwa…

SOCIALIZE

twitterfacebookgoogle plusemail

IN CASE YOU MISSED IT

FOR INSURANCE SERVICES CLICK HERE