mwananchi, Nyrere Foundation
Joseph Butiku, Mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya Mwalim Nyerere
“Mchakato huu una mambo makuu mawili ya kuamua ambayo ni kura ya Ndiyo au Hapana. Hivyo basi kupiga kura ya Hapana siyo dhambi kwani inatoa nafasi kwetu sote kukaa tena na kuangalia upungufu uliojitokeza na kilichosababisha upungufu huo nini ili tusirudie tena makosa,” alisema Butiku na kuongeza:

“Kura ya ndiyo inamaanisha tunaikubali Katiba Inayopendekezwa, hata ikiwa haina mashiko itaendelea kutumika kwa vile mmeikubali, lakini nisisitize kwamba kura ya hapana siyo dhambi, ipo kisheria na asije mtu akawaambia mpigie kura ya ndiyo.


Alisema kabla ya kuipitisha au kuikataa Katiba Inayopendekezwa ni vyema ikashindaniwa kwa hoja na si kwa nguvu au ngumi huku akiwataka vijana nchini kutothubutu kujiingiza kwenye mikumbo inayoweza kusababisha nchi ikaingia kwenye machafuko.

Aliyasema hayo kwenye mdahalo wa Katiba ulioandaliwa na taasisi hiyo ambao ulifanyika katika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Teofilo Kisanji (Teku) jijini Mbeya, Butiku alisema kura ya Hapana au Ndiyo, zote zinatoa fursa sawa kwa wananchi kuamua kwa utashi wao.
Katika mkutano huo uliohudhuriwa na mamia ya wakazi wa Mbeya, Butiku aliyekuwa Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliyoongozwa na Jaji Joseph Warioba, alieleza kuwashangaa viongozi wa vyama na Serikali kuwachagulia wananchi kura ya Ndiyo.

Akitolea mfano wa chama chake cha CCM, Butiku alisema hakitakiwi kuwahadaa Watanzania na kuwataka kuipigia kura ya Ndiyo katiba hiyo, badala yake kiwaache waamue wenyewe.
Aliwataka wananchi watumie muda huu kuitafuta nakala ya Katiba Inayopendekezwa, waisome na kuielewa ili hatimaye waamue ama kuipigia kura ya Hapana au Ndiyo.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

SOCIALIZE

twitterfacebookgoogle plusemail

IN CASE YOU MISSED IT

FOR INSURANCE SERVICES CLICK HERE