mwananchi, Nyrere Foundation
Joseph Butiku, Mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya Mwalim Nyerere
“Mchakato huu una mambo makuu mawili ya kuamua ambayo ni kura ya Ndiyo au Hapana. Hivyo basi kupiga kura ya Hapana siyo dhambi kwani inatoa nafasi kwetu sote kukaa tena na kuangalia upungufu uliojitokeza na kilichosababisha upungufu huo nini ili tusirudie tena makosa,” alisema Butiku na kuongeza:

“Kura ya ndiyo inamaanisha tunaikubali Katiba Inayopendekezwa, hata ikiwa haina mashiko itaendelea kutumika kwa vile mmeikubali, lakini nisisitize kwamba kura ya hapana siyo dhambi, ipo kisheria na asije mtu akawaambia mpigie kura ya ndiyo.


Alisema kabla ya kuipitisha au kuikataa Katiba Inayopendekezwa ni vyema ikashindaniwa kwa hoja na si kwa nguvu au ngumi huku akiwataka vijana nchini kutothubutu kujiingiza kwenye mikumbo inayoweza kusababisha nchi ikaingia kwenye machafuko.

Aliyasema hayo kwenye mdahalo wa Katiba ulioandaliwa na taasisi hiyo ambao ulifanyika katika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Teofilo Kisanji (Teku) jijini Mbeya, Butiku alisema kura ya Hapana au Ndiyo, zote zinatoa fursa sawa kwa wananchi kuamua kwa utashi wao.
Katika mkutano huo uliohudhuriwa na mamia ya wakazi wa Mbeya, Butiku aliyekuwa Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliyoongozwa na Jaji Joseph Warioba, alieleza kuwashangaa viongozi wa vyama na Serikali kuwachagulia wananchi kura ya Ndiyo.

Akitolea mfano wa chama chake cha CCM, Butiku alisema hakitakiwi kuwahadaa Watanzania na kuwataka kuipigia kura ya Ndiyo katiba hiyo, badala yake kiwaache waamue wenyewe.
Aliwataka wananchi watumie muda huu kuitafuta nakala ya Katiba Inayopendekezwa, waisome na kuielewa ili hatimaye waamue ama kuipigia kura ya Hapana au Ndiyo.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
  • JAMES LEMBELI AONDOKA CCM
    James Lembeli James Lembeli, Mbunge wa Kahama aliyemaliza muda wake amekataa kubadili msimamo wake wa…
  • ACT - TANZANIA vs ACT-WAZALENDO
    ACT-TANZANIA ACT-TANZANIA DHIDI YA ACT-WAZALENDO ACT-WAZALENDO Zitto alijiunga…
  • 2015 ACSEE EXAMINATION RESULTS
    Matokeo ya Kidato cha Sita yametangazwa rasmi na Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA). MATOKEO YA KIDATO…
  • MARIJUANA WORTH TSH 30 MILLION BURNT
    Nebuye village, Ukerewe. On Thursday members of the District Defense and Security Committee uprooted and…
  • ACACIA TAX FEUD: EXECUTIVE CHAIRMAN MET WITH TANZANIA PRESIDENT
    Tanzania’s President met with Barrick Gold Corp. Executive Chairman John Thornton in an effort to…
  • 9 DECEMBER 2015 UHURU DAY CANCELLED - MAGUFULI
    President John Magufuli has ordered the cancellation of 9th December 2015 Independence Day Celebrations for…
  • UHURU IN COURT OVER WAIGURU SAGA
    Raila Odinga is demanding President Uhuru Kenyatta be summoned as a witness in his legal duel with…
  • ARMY LAND CRUISER STOLEN
    Kenya; There is mystery surrounds the disappearance of a Kenya Army Land Cruiser from the Embakasi…
  • KITUO CHA RADIO KILICHOTANGAZA MAPINDUZI YA BURUNDI CHACHOMWA MOTO
    Kituo cha Radio Burundi …
  • DANGOTE KUJENGA BANDARI YAKE MTWARA
    Alhaji Dangote akisikiliza maelezo ya eneo husika Mtwara Wakazi wa kijiji cha Mgao, kata Naumbu…

SOCIALIZE

twitterfacebookgoogle plusemail

IN CASE YOU MISSED IT

FOR INSURANCE SERVICES CLICK HERE