Mahakama kuu ya Tanzania imepokea msaada wa mashine 38 za kupiga chapa Kutoka Mahakama ya mauaji ya Kimbari(ICTR) itakayorahisisha upatikanaji wa nakala za hukumu na mwenendo wa kesi mbalimbali hapa nchini.

Akipokea Msaada huo Jaji Mkuu wa Tanzania Mohammed Chande Othman alisema kuwa msaada huo utasaidia upatikanaji wa haki kuwa rahisi pia, kwani umekuja wakati muafaka wakati mahakama ikiwa katika mabadiliko ya kuzifanya kesi kwenda kwa wakati.
Jaji Othman alisema changamoto ya utoaji haki kwa wakati imeweza kurahisishwa kwa upatikanaji wa mashine hizo ambazo ni za kisasa na za gharama ambazo zimeipunguzia mzigo serikali.

“Mashine hizi za msaada  baada ya kupatikana sasa ni mwendelezo wa mashirikiano yetu kati ya serikali na mahakama hii ikiwemo ukamataji wa wahalifu, kuwatunza na kuwalinda hivyo ni moja ya faida za mashirikiano hayo”alisema Jaji Mkuu.
Alisema kuwa ushirikiano uliopo kati ya mahakama ya kimataifa ya mauaji ya kimbari na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni wa muda mrefu kuanzia kwenye ukamataji wa wahalifu wa mauji hadi kuwahifadhi hivyo hii sehemu ya mashirikiano hayo ya muda mrefu.

Jaji Othman alisema kuwa Hatua ya msaada huo itaendana vizuri na ufundishaji wa makatibu wetu ilikuweza kufanyakazi kiufanisi kwa kutumia msaada huo wa vitendea kazi hivyo akaiomba mahakama hiyo kuendana na mbio za kiutendaji ili kufanikisha upatikanaji haki kwa wakati.

Mashine hizo zenye thamani ya dolla 95,000 zimetolewa na mahakama ya mauaji ya Kimbari kwa mahakama yetu ili ziwezekusaidia kupunguza malalamiko na uchelewaji wa kutoa nakala za hukumu na mwenendo wa kesi za jinai hapa nchini.

“Vitendeakazi hivi vimekuja wakati muafaka kwani tumekuwa katika mikakati ya ubadilishaji wa utumiaji wa kuandikia mikono kwenda kwenye utumiaji wa vifaa kutakakorahisisha kutoa hukumu na mwenendo wa kesi kwa wakati na kuacha kutumia muda mrefu kupata nakala za hukumu na mwenendo wa kesi mbalimbali” alisema Jaji Othman.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
  • KIKWETE ORDERED TAX EXEMPTION ON CONTAINERS
    Former President of Tanzania has dismissed allegations that he sanctioned the removal of containers from…
  • 15 PATIENTS WITH CHOLERA IN MWANZA AND 7 IN KIGOMA, TANZANIA
    Mwanza. Cholera outbreak in Mwanza Region has been contained tremendously with current statistics showing…
  • IS YAMCHOMA MOTO RUBANI WA JORDAN HADI KUFA
    Serikali ya Jordan imesema itachukua hatua kali za kulipiza kisasi kufuatia kundi la IS kutoa…
  • ZITTO KABWE AHAMIA ACT-TANZANIA
    ZITTO KABWE Siasa za Tanzania kwa hivi sasa zimechukua mkondo mpya baada ya aliyekuwa mbunge wa Kigoma…
  • MAGAZETI YA LEO
    Kama kawaida Habari Duniani inakupa vichwa vya habari vya magazeti yote ya kila siku. Leo pia…
  • 1300 EMPLOYEES TO BE LAID OFF BEFORE 2016
    Mwanza, Tanzania: The ACACIA God Mine is expected to lay off 1300 employees before the end of this year.…
  • 5 BORA YA CCM URAISI 2015
    CCM imeyatangaza majina matano yaliyopitishwa na Kamati ya CCM (CC) MAJINA MATANO 1. Bernard Membe 2.…
  • TANZANIA YAFUZU KUCHEZA KOMBE LA DUNIA
    Baada ya kufungwa na Kenya, timu ya Tanzania imeibuka na kuifunga Nigeria kwa wiketi tatu katika mwendelezo…
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2014 - TANZANIA CSEE 2014 RESULT
    MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2014 BOFY HAPA CSEE 2014 RESULT CLICK HERE
  • ZITTO KABWE AHAMIA ACT-TANZANIA
    ZITTO KABWE Siasa za Tanzania kwa hivi sasa zimechukua mkondo mpya baada ya aliyekuwa mbunge wa Kigoma…

SOCIALIZE

twitterfacebookgoogle plusemail

IN CASE YOU MISSED IT

FOR INSURANCE SERVICES CLICK HERE