Mahakama kuu ya Tanzania imepokea msaada wa mashine 38 za kupiga chapa Kutoka Mahakama ya mauaji ya Kimbari(ICTR) itakayorahisisha upatikanaji wa nakala za hukumu na mwenendo wa kesi mbalimbali hapa nchini.

Akipokea Msaada huo Jaji Mkuu wa Tanzania Mohammed Chande Othman alisema kuwa msaada huo utasaidia upatikanaji wa haki kuwa rahisi pia, kwani umekuja wakati muafaka wakati mahakama ikiwa katika mabadiliko ya kuzifanya kesi kwenda kwa wakati.
Jaji Othman alisema changamoto ya utoaji haki kwa wakati imeweza kurahisishwa kwa upatikanaji wa mashine hizo ambazo ni za kisasa na za gharama ambazo zimeipunguzia mzigo serikali.

“Mashine hizi za msaada  baada ya kupatikana sasa ni mwendelezo wa mashirikiano yetu kati ya serikali na mahakama hii ikiwemo ukamataji wa wahalifu, kuwatunza na kuwalinda hivyo ni moja ya faida za mashirikiano hayo”alisema Jaji Mkuu.
Alisema kuwa ushirikiano uliopo kati ya mahakama ya kimataifa ya mauaji ya kimbari na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni wa muda mrefu kuanzia kwenye ukamataji wa wahalifu wa mauji hadi kuwahifadhi hivyo hii sehemu ya mashirikiano hayo ya muda mrefu.

Jaji Othman alisema kuwa Hatua ya msaada huo itaendana vizuri na ufundishaji wa makatibu wetu ilikuweza kufanyakazi kiufanisi kwa kutumia msaada huo wa vitendea kazi hivyo akaiomba mahakama hiyo kuendana na mbio za kiutendaji ili kufanikisha upatikanaji haki kwa wakati.

Mashine hizo zenye thamani ya dolla 95,000 zimetolewa na mahakama ya mauaji ya Kimbari kwa mahakama yetu ili ziwezekusaidia kupunguza malalamiko na uchelewaji wa kutoa nakala za hukumu na mwenendo wa kesi za jinai hapa nchini.

“Vitendeakazi hivi vimekuja wakati muafaka kwani tumekuwa katika mikakati ya ubadilishaji wa utumiaji wa kuandikia mikono kwenda kwenye utumiaji wa vifaa kutakakorahisisha kutoa hukumu na mwenendo wa kesi kwa wakati na kuacha kutumia muda mrefu kupata nakala za hukumu na mwenendo wa kesi mbalimbali” alisema Jaji Othman.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
  • IS YAMCHOMA MOTO RUBANI WA JORDAN HADI KUFA
    Serikali ya Jordan imesema itachukua hatua kali za kulipiza kisasi kufuatia kundi la IS kutoa…
  • SMUGGLER'S IMPOUNDED TANZANITE AUCTIONED IN ARUSHA GEM FAIR
    Arusha. Tanzanite gemstones valued at more than 2.5 billion/- were auctioned during the recently held Arusha…
  • MARIJUANA WORTH TSH 30 MILLION BURNT
    Nebuye village, Ukerewe. On Thursday members of the District Defense and Security Committee uprooted and…
  • TODAY NEWSPAPER FRONT PAGES - TANZANIA
    Today Tanzania newspapers HabariDuniani brings Tanzania newspaper headlines at your finger tips. THE…
  • AN AFRICAN MAN SOLVES A 270 YEARS OLD MATH PROBLEM
    AN AFRICAN MAN SOLVES A 270 YEARS OLD MATH PROBLEM Ibrahima Sambégou Diallo may have become the…
  • WATOTO WAFICHWA NA KUPATIWA MAFUNZO YA KIISLAM KWA SIRI
  • THIERRY HENRY WOMAN LOOK IN WALES
    THIERRY HENRY THIERRY HENRY AVAA WIGI Aliyekuwa mshambulizi mahiri aliyewai kuchezea timu ya Arsenal ya…
  • GOOGLE SALUTES TANZANIA INDEPENDENCE DAY
    GOOGLE has saluted Tanzanians on the Independence celebration by removing one O and put the nation…
  • World's Richest person according to Forbes 2015
    Carlos Slim Helu …
  • ARUMERU: WANANCHI WAVAMIA SHAMBA LA MWEKEZAJI LA KARATU ESTATE
    WANANCHI WAVAMIA SHAMBA LA MWEKEZAJI Yafuatayo ni baaadhi ya mabango yaliyokutwa katika Karamu Estate…

SOCIALIZE

twitterfacebookgoogle plusemail

IN CASE YOU MISSED IT

FOR INSURANCE SERVICES CLICK HERE