Mahakama kuu ya Tanzania imepokea msaada wa mashine 38 za kupiga chapa Kutoka Mahakama ya mauaji ya Kimbari(ICTR) itakayorahisisha upatikanaji wa nakala za hukumu na mwenendo wa kesi mbalimbali hapa nchini.

Akipokea Msaada huo Jaji Mkuu wa Tanzania Mohammed Chande Othman alisema kuwa msaada huo utasaidia upatikanaji wa haki kuwa rahisi pia, kwani umekuja wakati muafaka wakati mahakama ikiwa katika mabadiliko ya kuzifanya kesi kwenda kwa wakati.
Jaji Othman alisema changamoto ya utoaji haki kwa wakati imeweza kurahisishwa kwa upatikanaji wa mashine hizo ambazo ni za kisasa na za gharama ambazo zimeipunguzia mzigo serikali.

“Mashine hizi za msaada  baada ya kupatikana sasa ni mwendelezo wa mashirikiano yetu kati ya serikali na mahakama hii ikiwemo ukamataji wa wahalifu, kuwatunza na kuwalinda hivyo ni moja ya faida za mashirikiano hayo”alisema Jaji Mkuu.
Alisema kuwa ushirikiano uliopo kati ya mahakama ya kimataifa ya mauaji ya kimbari na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni wa muda mrefu kuanzia kwenye ukamataji wa wahalifu wa mauji hadi kuwahifadhi hivyo hii sehemu ya mashirikiano hayo ya muda mrefu.

Jaji Othman alisema kuwa Hatua ya msaada huo itaendana vizuri na ufundishaji wa makatibu wetu ilikuweza kufanyakazi kiufanisi kwa kutumia msaada huo wa vitendea kazi hivyo akaiomba mahakama hiyo kuendana na mbio za kiutendaji ili kufanikisha upatikanaji haki kwa wakati.

Mashine hizo zenye thamani ya dolla 95,000 zimetolewa na mahakama ya mauaji ya Kimbari kwa mahakama yetu ili ziwezekusaidia kupunguza malalamiko na uchelewaji wa kutoa nakala za hukumu na mwenendo wa kesi za jinai hapa nchini.

“Vitendeakazi hivi vimekuja wakati muafaka kwani tumekuwa katika mikakati ya ubadilishaji wa utumiaji wa kuandikia mikono kwenda kwenye utumiaji wa vifaa kutakakorahisisha kutoa hukumu na mwenendo wa kesi kwa wakati na kuacha kutumia muda mrefu kupata nakala za hukumu na mwenendo wa kesi mbalimbali” alisema Jaji Othman.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
  • ACACIA TAX FEUD: EXECUTIVE CHAIRMAN MET WITH TANZANIA PRESIDENT
    Tanzania’s President met with Barrick Gold Corp. Executive Chairman John Thornton in an effort to…
  • HAVE YOU READ TODAY UK FRONT PAGES NEWSPAPER? READ NOW
    HabaruDuniani brings to you UK front pages Newspaper at your finger tips. Please do not forget to like our…
  • MAGUFULI SACK TANZANIA ANTI-CORRUPTION BODY CHIEF DR.HOSEAH
    Tanzania President Dr. Magufuli sacks Director General of The Prevention and Combating of Corruption…
  •  *TANZANIA'S HOME AFFAIRS MINISTER SUSPENDED FOR ALCOHOLISM
    President John Magufuli of Tanzania has revoked appointment of Home Affair Minister Charles Kitwanga for…
  • Maandamano ya Kigoma yampa Ujumbe huu Dk.Slaa wa CHADEMA
    Ujumbe wa Dk.Slaa kutoka Kigoma …
  • PLANE CARRYING 58 PASSENGERS CRASH
    A Taiwanese passenger aircraft with 58 people on board has crashed into a river outside Taiwan’s capital…
  • MAWAZIRI NA VIGOGO WALIOSHINDWA KURA ZA MAONI CCM
    Mathias Chikawe Waziri wa Mambo ya ndani ni miongoni mwa wanachama maarufu wa CCM walioshindwa…
  • BUTIKU: CHAMA CHANGU (CCM) MAGWIJI WA KUVUNJA TARATIBU (KATIBA)
    Joseph Butiku,Mkurugenzi wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere Joseph Butiku,Mkurugenzi wa Taasisi ya Mwalimu…
  • KWA NINI HIZI SHULE ZIMEPEWA HAYA MAJINA?
    SHULE YA MSINGI MADUDU SHULE YA MSINGI KITOBO SHULE YA MSINGI MKUNWA SHULE YA MSINGI…
  • NESI AMCHAPA VIBOKO MJAMZITO NA MTOTO AFIA TUMBONI
    MANESI WAKISHIRIKISHANA JAMBO Muuguzi aliyekuwa zamu katika kituo cha Afya cha Muungano wilayani…

SOCIALIZE

twitterfacebookgoogle plusemail

IN CASE YOU MISSED IT

FOR INSURANCE SERVICES CLICK HERE