Dk Titus Kamani ashindwa uchaguzi

Hali ilikuwa mbaya jimboni Busega ambako baada ya Dk Kamani na wafuasi walizuia matokeo kutangazwa na kuibuka kwa vurugu zilizosababisha polisi kuingilia kati na kukamata watu wanne walioonekana kumuunga mkono.

Matokeo ya Jimbo la Busega yamekwama baada ya Waziri wa Uvuvi na Maendeleo ya Mifugo, Dk Titus Kamani kumshambulia msimamizi wa uchaguzi, baada ya kutangazwa matokeo kua ameshindwa.

Mawaziri wengine walioshindwa, Bofya hapa

Dk. Chegeni ambwaga Dk.Kamani

Halmashauri Kuu ya CCM iliagiza kurudiwa kwa kura za maoni za ubunge kwenye jimbo hilo baada ya kubaini kuwa kulikuwa na ukiukwaji wa kanuni. Katika kura za Awali, Dk Kamani na Dk Chegeni, kila mmoja kwa wakati wake alijitangaza kuwa mshindi, lakini baada ya matokeo rasmi kutangaza Dk Chegeni aliibuka mshindi kwa kupata kura 13,048 dhidi ya 11,829 za Dk Kamani.


“Napigania haki yangu,” alisema Dk Kamani baada ya kutulia kwa vurugu ambazo zilihusisha kupigwa kwa msimamizi wa kura hizo za maoni, Jonathan Mabiya.
“Huu ni ushindani. Uchaguzi uliopita tulikubaliana na matokeo na tulisaini, lakini uongozi umesema turudie, leo hatujasaini wanataka kutangaza kwa nguvu, hatujakubaliana.”

Mkuu wa Wilaya ya Busega, Paul Mzindakaya, licha ya matokeo kutotatangazwa alisema watu hawana budi kukubaliana na matokeo na kusema kitendo cha Dk Kamani kwa kuhusika kwenye vurugu hizo ni cha kibinadamu.

“Aliyeshinda ameshinda tu hakuna namna. Kilichofanywa na Waziri Kamani kumpiga msimamizi huyo ni mambo ya binadamu tu… lakini walioshindwa lazima wakubali matokeo na lazima yatangazwe,” alisema Mzindakaya.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
  • UHURU IN COURT OVER WAIGURU SAGA
    Raila Odinga is demanding President Uhuru Kenyatta be summoned as a witness in his legal duel with…
  • Maandamano ya Kigoma yampa Ujumbe huu Dk.Slaa wa CHADEMA
    Ujumbe wa Dk.Slaa kutoka Kigoma …
  • Amazing Vehicles manufactured in Tanzania, East Afrika - Nyumbu
    Nyumbu A number of African countries chose  institutions of higher learning like universities to…
  • GLOBAL ENTREPRENEURSHIP SUMMIT IN NAIROBI, KENYA 2015
    WHAT IS GLOBAL ENTREPRENEURSHIP SUMMIT IN NAIROBI 2015? The Global Entrepreneurship Summit (GES) Youth…
  • Relationship between Arsenal and Manchester City
    Arsenal and Manchester City have had numerous connections over the past 30 years, especially with a…
  • NAFASI ZA KAZI BENKI KUU YA TANZANIA
    EMPLOYMENT OPPORTUNITY AT BANK OF TANZANIA The bank of Tanzania, an equal opportunity employer and…
  • 32 DEAD, 80 WOUNDS IN YOLA, NIGERIA EXPLOSION
    Yola, Nigeria. An explosion occurred in the city of Yola, Nigeria. The night-time blasts ripped through…
  • SMUGGLER'S IMPOUNDED TANZANITE AUCTIONED IN ARUSHA GEM FAIR
    Arusha. Tanzanite gemstones valued at more than 2.5 billion/- were auctioned during the recently held Arusha…
  • MAGAZETI YA LEO
    Kama kawaida Habari Duniani inakupa vichwa vya habari vya magazeti yote ya kila siku. Leo pia…
  • MAHAKAMA TANZANIA YAPOKEA MSAADA WENYE THAMANI YA DOLLA 95,000
    Mahakama kuu ya Tanzania imepokea msaada wa mashine 38 za kupiga chapa Kutoka Mahakama ya mauaji ya…

SOCIALIZE

twitterfacebookgoogle plusemail

IN CASE YOU MISSED IT

FOR INSURANCE SERVICES CLICK HERE