Majimbo hayo yalitangazwa na wawakilishi wa makatibu wakuu wa UKAWA, John Mnyika (Chadema), Nderakindo Kessy (NCCR – Mageuzi), Shaweji Mketo (CUF) na Masudi Makujunga (NLD) waliokutana katika Ofisi za Makao Makuu ya za NCCR – Mageuzi.

Majimbo waliogawana UKAWA

253 ni majimbo ambayo yamegawanywa na Vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kati ya majimbo 265 ya ubunge huku 12 yaliyokuwa kwenye mvutano yakibaki kiporo.
John Mnyika (Chadema), Nderakindo Kessy (NCCR – Mageuzi), Shaweji Mketo (CUF) na Masudi Makujunga (NLD)

Majimbo ya UKAWA

Miongoni mwa majimbo ambayo hayajagawanywa ni, Segerea, Kigamboni, Mbarali, Geita Vijijini, Gairo, Mtwara, Mpwapwa na Geita Mjini, Mwanga na Serengeti ambalo Katibu Mkuu wa NCCR – Mageuzi, Mosena Nyambabe jana alichukua fomu kuliwania.

Katika mgawanyo huo uliotangazwa kwa wanahabari jana, Chadema kimepata majimbo 138, sawa na asilimia 73 ya majimbo yote huku CUF ikichukua majimbo 99, NCCR – Mageuzi majimbo 14 na NLD majombo matatu.
Hiyo ni pamoja na kujumlisha majimbo 51 ya Zanzibar ambayo yote yalikwenda kwa CUF isipokuwa moja lililoachwa kwa Chadema.

Takwimu za Uchaguzi

Chadema ambacho katika uchaguzi uliopita kilipata majimbo 24 dhidi ya manne ya NCCR-Mageuzi na mawili ya CUF Bara, kimeachiwa majimbo karibu yote katika mikoa ya Mara, Shinyanga, Geita, Njombe, Rukwa, Arusha, Manyara, Singida, Katavi huku Cuf ikibeba mkoa wote wa Lindi na NCCR-Mageuzi ikibeba ngome ya Kigoma.
Katika mgawanyo huo, NLD ambayo haikuwa na jimbo hata moja imeachiwa majimbo matatu tu ya Lulindi, Masasi na Ndanda mkoani Mtwara.

Wawakilishi wa makatibu wakuu wa UKAWA walisema uamuzi huo umefikiwa baada ya majadiliano ya muda mrefu, kuhusu kuachiana majimbo ya ubunge kwa vyama vinavyounda UKAWA.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

SOCIALIZE

twitterfacebookgoogle plusemail

IN CASE YOU MISSED IT

FOR INSURANCE SERVICES CLICK HERE