Majimbo hayo yalitangazwa na wawakilishi wa makatibu wakuu wa UKAWA, John Mnyika (Chadema), Nderakindo Kessy (NCCR – Mageuzi), Shaweji Mketo (CUF) na Masudi Makujunga (NLD) waliokutana katika Ofisi za Makao Makuu ya za NCCR – Mageuzi.

Majimbo waliogawana UKAWA

253 ni majimbo ambayo yamegawanywa na Vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kati ya majimbo 265 ya ubunge huku 12 yaliyokuwa kwenye mvutano yakibaki kiporo.
John Mnyika (Chadema), Nderakindo Kessy (NCCR – Mageuzi), Shaweji Mketo (CUF) na Masudi Makujunga (NLD)

Majimbo ya UKAWA

Miongoni mwa majimbo ambayo hayajagawanywa ni, Segerea, Kigamboni, Mbarali, Geita Vijijini, Gairo, Mtwara, Mpwapwa na Geita Mjini, Mwanga na Serengeti ambalo Katibu Mkuu wa NCCR – Mageuzi, Mosena Nyambabe jana alichukua fomu kuliwania.

Katika mgawanyo huo uliotangazwa kwa wanahabari jana, Chadema kimepata majimbo 138, sawa na asilimia 73 ya majimbo yote huku CUF ikichukua majimbo 99, NCCR – Mageuzi majimbo 14 na NLD majombo matatu.
Hiyo ni pamoja na kujumlisha majimbo 51 ya Zanzibar ambayo yote yalikwenda kwa CUF isipokuwa moja lililoachwa kwa Chadema.

Takwimu za Uchaguzi

Chadema ambacho katika uchaguzi uliopita kilipata majimbo 24 dhidi ya manne ya NCCR-Mageuzi na mawili ya CUF Bara, kimeachiwa majimbo karibu yote katika mikoa ya Mara, Shinyanga, Geita, Njombe, Rukwa, Arusha, Manyara, Singida, Katavi huku Cuf ikibeba mkoa wote wa Lindi na NCCR-Mageuzi ikibeba ngome ya Kigoma.
Katika mgawanyo huo, NLD ambayo haikuwa na jimbo hata moja imeachiwa majimbo matatu tu ya Lulindi, Masasi na Ndanda mkoani Mtwara.

Wawakilishi wa makatibu wakuu wa UKAWA walisema uamuzi huo umefikiwa baada ya majadiliano ya muda mrefu, kuhusu kuachiana majimbo ya ubunge kwa vyama vinavyounda UKAWA.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
  • FREE EDUCATION IN TANZANIA
    Tanzania government has released a circular detailing how the new free education policy will be…
  • APANDIKIZWA UUME
    Daktari wa usapuaji nchini Afrika Kusini amethibitisha kwamba mwanamme wa kwanza aliyepandikizwa uume…
  • 32 DEAD, 80 WOUNDS IN YOLA, NIGERIA EXPLOSION
    Yola, Nigeria. An explosion occurred in the city of Yola, Nigeria. The night-time blasts ripped through…
  • Vehicles manufactured in West Afrika
    The Kantanka is a car that was conceived, designed and made in Ghana. This brand of cars is probably the…
  • ACT - TANZANIA vs ACT-WAZALENDO
    ACT-TANZANIA ACT-TANZANIA DHIDI YA ACT-WAZALENDO ACT-WAZALENDO Zitto alijiunga…
  • AJALI YA TRENI NA LORI
    AJALI …
  • SUMAYE AJIUNGA UKAWA BAADA YA KUHAMA CCM
    Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Serikali ya awamu ya tatu Mhe. Frederick Sumaye kujivua uanachana na kujiunga na…
  • Tanzania launches Sustainable Energy for All SE4ALL
    Dar es Salaam, Tanzania launches Sustainable Energy for All (SE4ALL) today at Julius Nyerere International…
  • 3 MILLIONS CROWDS PROTEST AGAINST BRAZIL'S PRESIDENT
    Widespread Anger against Brazilian President Dilma Rousseff is mounting as hundreds of thousands of people…
  • Wananchi wa Mwanza Wabomoa ujenzi wa Mtaa wa Makoroboi
    Wananchi wakiboboa Nguzo katika mtaa wa Makoroboi, Mwanza Normal 0 false false …

SOCIALIZE

twitterfacebookgoogle plusemail

IN CASE YOU MISSED IT

FOR INSURANCE SERVICES CLICK HERE