Waziri Mkuu Mizengo Pinda

UPINZANI KUCHUKUA DOLA

Chama chochote cha siasa nchini kina nafasi ya kushika dola endapo kitafuata kanuni na taratibu zilizowekwa na mamlaka husika, alisema Waziri Mkuu msataafu Dk. Salim Ahmed Salim
Waziri mkuu mstaafu, Dk Salim Ahmed Salim  akizungumza jijini Dar es Salaam jana wakati wa ufunguzi wa Semina ya Urithi na Utamaduni wa Tanzania. Kushoto ni mkurugenzi wa taasisi hiyo kutoka Chuo Kikuu cha Kiislamu Morogoro (MUM), Profesa Abdallah Bujra
“Utakuta viongozi wa vyama wenyewe kwa wenyewe wanarushiana maneno, huyu hafai  mara siyo raia wa nchi hii, sasa haya mambo kwenye siasa hayatakiwi.

“Ni lazima kila kiongozi wa chama cha siasa atambue wajibu  wake katika jamii,”
Pia maadili ya viongozi katika Taifa yameporomoka,  hivyo aliwaasa wananchi kuchagua viongozi bora kwa masilahi ya Taifa katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25 mwaka huu.

“Sasa kiongozi anagombea nafasi fulani kwa masilahi yake binafsi, siyo kwa wananchi  na anawaomba wampigie kura,” alisema Dk Salim.
Dk Salim alisema hayo jana baada ya kufungua semina iliyoandaliwa na Taasisi ya Utamaduni na Urithi kutoka Chuo Kikuu cha Kiislamu Morogoro (MUM).
Aliwataka wananchi kuwa watulivu  na kuilinda amani katika kipindi hiki cha uchaguzi.

Katika semina hiyo ya Urithi na Utamaduni wa Tanzania alisema nchi ina urithi lakini haujapewa kipaumbele.
Mkurugenzi wa taasisi hiyo, Profesa Abdallah Bujra alisema semina hiyo itakuwa ya siku tatu.

Alisema Taifa haliwezi kupiga hatua bila suala hilo kutiliwa mkazo.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

SOCIALIZE

twitterfacebookgoogle plusemail

IN CASE YOU MISSED IT

FOR INSURANCE SERVICES CLICK HERE