tanzania, Viongozi wa Dini
Raisi Kikwete alipozungumza na baadhi ya viongozi wa Dini
Katika tamko la pamoja walilolitoa baada ya kukutana mjini Dodoma, viongozi hao (maaskofu) wamemtahadharisha Rais Kikwete kuwa kuendelea kupigia debe Katiba Inayopendekezwa na kuruhusu Mahakama ya Kadhi, kunaweza kulitumbukiza Taifa katika machafuko na hali ikiwa hivyo Serikali ndiyo itakayolaumiwa.

Tamko hilo limesainiwa na viongozi walewale waliosaini lile la awali la Machi 12, mwaka huu ambao ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT), Askofu Dk Alex Malasusa, Mwenyekiti wa Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki Tanzania (TEC), Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa na Mwenyekiti wa Kanisa la Pentekoste Tanzania (CPCT), Askofu Daniel Awet.

Tamko hilo la maneno 921, limeendelea kuwataka waumini wao kujitokeza kwa wingi kujiandikisha katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, kuisoma Katiba Inayopendekezwa na kujitokeza kuikataa kwa kupiga kura ya ‘hapana,’ msimamo ambao tayari umeibua msuguano baina yao na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo aliyesema viongozi wa dini hawana mamlaka ya kuwaamulia waumini wao aina ya kura wanayostahili kupiga.

Pia, Jukwaa hilo limewataka viongozi wakuu wa Serikali –Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Rais Kikwete wasifurahi kwamba ujumbe wao umewafikia viongozi wa dini waliozungumza nao hivi karibuni, kwa kuwa watu waliokutana nao si wawakilishi rasmi na hawana uwezo wa kutoa uamuzi au kukubaliana juu ya jambo la kitaifa.

“Maaskofu tuliokutana hapa (mjini Dodoma) hatuna hasira na wala hatuongozwi na hasira wala mihemko katika kufikia maamuzi tunayofanya kama ambavyo wengine wanavyotutafsiri, tunafikia maamuzi yetu baada ya maombi na sala na tunasukumwa na upendo kwa wananchi ili kujenga Taifa lenye umoja, amani, utulivu na maelewano,” lilisema tamko hilo likihitimishwa kwa maneno ya Biblia kutoka Mithali 29: 1, “Aonywaye mara nyingi akishupaza shingo, atavunjika ghafla, wala hapati dawa.”

“Muswada huu unapendekeza kuanzishwa Mahakama ya Kadhi ambao utawasilishwa bungeni leo kwa hati ya dharura na hivyo kuufanya umma wa Watanzania kutokujua maudhui yaliyomo katika muswada huo wakati bado hoja zetu za msingi tulizopeleka kwenye Kamati ya Katiba na Sheria ya Bunge na kwa Waziri Mkuu hazijajibiwa,” Ilieleza taarifa hiyo.

“Tunamtaka Rais aagize muswada huu uondolewe bungeni na usijadiliwe tena kwa kuwa utafiti wa Tume ya kurekebisha sheria ulishaonyesha madhara ya uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi. Vinginevyo, kuendelea kujadiliwa kwa muswada huu maana yake ni kwamba Serikali inajihusisha na itagharimia mahakama hiyo.”

Walisema; “Yalijitokeza kwenye semina kwa wabunge mwishoni mwa wiki ni ishara ndogo ya kile kitakachotokea maeneo yote ya nchi yetu. Hapa tunajiuliza, endapo maneno ya Rais ni kweli, mbona Bunge linaendelea kujadili kitu ambacho Serikali haitajihusisha wala kukigharamia?”

Tamko hilo lilionya: “Tunamtaka Rais (Kikwete) aiepushe nchi yetu na kuingizwa kwenye mapigano ya kidini ambayo kuyadhibiti itakuwa vigumu. Pia tunamwomba Rais Kikwete akumbuke na kutafakari kile kilichotokea na kinachotokea nchi ya Afrika ya Kati, kati ya kundi la Seleka na kundi la Anti Balaka.

Jumamosi iliyopita, Rais Kikwete akifungua mkutano wa Kamati ya Amani ya Mkoa wa Dar es Salaam iliyoshirikisha wajumbe kutoka mikoa mbalimbali ikijumuisha viongozi wa dini za Kiislamu na Kikristo, alisema msimamo wa TCF kuhusu kuipigia kura ya ‘hapana’ Katiba Inayopendekezwa ni wa hasira na usiokuwa na tija kwa maendeleo ya Taifa.

Rais Kikwete alisema: “Waacheni waumini waamue Katiba wanayoitaka wao... hayo matamko niliyoyasoma yamejaa hasira kwa Serikali kupeleka bungeni Muswada wa Mahakama ya Kadhi.”

“Nimeyasoma matamko hayo yote kwa umakini, imenishangaza, imenisikitisha na kunihuzunisha. Siamini kwa nini wamefikia huko kwa kuunga au kutokuunga mkono,” alisema Rais Kikwete. 

Nini maoni yako kuhusu hili swala? Washirikishe wengine habari hii.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2014 - TANZANIA CSEE 2014 RESULT
    MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2014 BOFY HAPA CSEE 2014 RESULT CLICK HERE
  • MRI EQUIPMENT REPAIRED AT MUHIMBILI AFTER MAGUFULI VISIT
    Muhimbili National Hospital (File Photo) Muhimbili National Hospital (MNH) has announced that…
  • MUTHAURA APPOINTED AS KENYA'S CAPITAL MARKETS AUTHORITY CHIEF EXECUTIVE
    Kenya. Paul Muthaura has been appointed the Kenya's Capital Markets Authority (CMA) chief executive, nearly…
  • MUSWADA WA AJIRA WAPITISHWA BUNGENI, TANZANIA
    Bunge la Tanzania Bunge la Tanzania limepitisha muswada wa sheria ya udhibiti wa ajira za wageni wa mwaka…
  • ACACIA TAX FEUD: EXECUTIVE CHAIRMAN MET WITH TANZANIA PRESIDENT
    Tanzania’s President met with Barrick Gold Corp. Executive Chairman John Thornton in an effort to…
  • SOMA MAGAZETI YA LEO HAPA
    Kama kawaida Habari Duniani inakupa vichwa vya habari vya magazeti yote ya kila siku. Leo pia…
  • MRI EQUIPMENT REPAIRED AT MUHIMBILI AFTER MAGUFULI VISIT
    Muhimbili National Hospital (File Photo) Muhimbili National Hospital (MNH) has announced that…
  • JAMES LEMBELI AONDOKA CCM
    James Lembeli James Lembeli, Mbunge wa Kahama aliyemaliza muda wake amekataa kubadili msimamo wake wa…
  • TANZANIA CABINET ANNOUNCED BY MAGUFULI
    Dar es Salaam. Tanzania President John Magufuli announced his cabinet of only 18 ministries led by 19…
  • MAGAZETI YA LEO
    Kama kawaida Habari Duniani inakupa vichwa vya habari vya magazeti yote ya kila siku. Leo pia…

SOCIALIZE

twitterfacebookgoogle plusemail

IN CASE YOU MISSED IT

FOR INSURANCE SERVICES CLICK HERE