tanzania, Viongozi wa Dini
Raisi Kikwete alipozungumza na baadhi ya viongozi wa Dini
Katika tamko la pamoja walilolitoa baada ya kukutana mjini Dodoma, viongozi hao (maaskofu) wamemtahadharisha Rais Kikwete kuwa kuendelea kupigia debe Katiba Inayopendekezwa na kuruhusu Mahakama ya Kadhi, kunaweza kulitumbukiza Taifa katika machafuko na hali ikiwa hivyo Serikali ndiyo itakayolaumiwa.

Tamko hilo limesainiwa na viongozi walewale waliosaini lile la awali la Machi 12, mwaka huu ambao ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT), Askofu Dk Alex Malasusa, Mwenyekiti wa Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki Tanzania (TEC), Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa na Mwenyekiti wa Kanisa la Pentekoste Tanzania (CPCT), Askofu Daniel Awet.

Tamko hilo la maneno 921, limeendelea kuwataka waumini wao kujitokeza kwa wingi kujiandikisha katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, kuisoma Katiba Inayopendekezwa na kujitokeza kuikataa kwa kupiga kura ya ‘hapana,’ msimamo ambao tayari umeibua msuguano baina yao na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo aliyesema viongozi wa dini hawana mamlaka ya kuwaamulia waumini wao aina ya kura wanayostahili kupiga.

Pia, Jukwaa hilo limewataka viongozi wakuu wa Serikali –Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Rais Kikwete wasifurahi kwamba ujumbe wao umewafikia viongozi wa dini waliozungumza nao hivi karibuni, kwa kuwa watu waliokutana nao si wawakilishi rasmi na hawana uwezo wa kutoa uamuzi au kukubaliana juu ya jambo la kitaifa.

“Maaskofu tuliokutana hapa (mjini Dodoma) hatuna hasira na wala hatuongozwi na hasira wala mihemko katika kufikia maamuzi tunayofanya kama ambavyo wengine wanavyotutafsiri, tunafikia maamuzi yetu baada ya maombi na sala na tunasukumwa na upendo kwa wananchi ili kujenga Taifa lenye umoja, amani, utulivu na maelewano,” lilisema tamko hilo likihitimishwa kwa maneno ya Biblia kutoka Mithali 29: 1, “Aonywaye mara nyingi akishupaza shingo, atavunjika ghafla, wala hapati dawa.”

“Muswada huu unapendekeza kuanzishwa Mahakama ya Kadhi ambao utawasilishwa bungeni leo kwa hati ya dharura na hivyo kuufanya umma wa Watanzania kutokujua maudhui yaliyomo katika muswada huo wakati bado hoja zetu za msingi tulizopeleka kwenye Kamati ya Katiba na Sheria ya Bunge na kwa Waziri Mkuu hazijajibiwa,” Ilieleza taarifa hiyo.

“Tunamtaka Rais aagize muswada huu uondolewe bungeni na usijadiliwe tena kwa kuwa utafiti wa Tume ya kurekebisha sheria ulishaonyesha madhara ya uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi. Vinginevyo, kuendelea kujadiliwa kwa muswada huu maana yake ni kwamba Serikali inajihusisha na itagharimia mahakama hiyo.”

Walisema; “Yalijitokeza kwenye semina kwa wabunge mwishoni mwa wiki ni ishara ndogo ya kile kitakachotokea maeneo yote ya nchi yetu. Hapa tunajiuliza, endapo maneno ya Rais ni kweli, mbona Bunge linaendelea kujadili kitu ambacho Serikali haitajihusisha wala kukigharamia?”

Tamko hilo lilionya: “Tunamtaka Rais (Kikwete) aiepushe nchi yetu na kuingizwa kwenye mapigano ya kidini ambayo kuyadhibiti itakuwa vigumu. Pia tunamwomba Rais Kikwete akumbuke na kutafakari kile kilichotokea na kinachotokea nchi ya Afrika ya Kati, kati ya kundi la Seleka na kundi la Anti Balaka.

Jumamosi iliyopita, Rais Kikwete akifungua mkutano wa Kamati ya Amani ya Mkoa wa Dar es Salaam iliyoshirikisha wajumbe kutoka mikoa mbalimbali ikijumuisha viongozi wa dini za Kiislamu na Kikristo, alisema msimamo wa TCF kuhusu kuipigia kura ya ‘hapana’ Katiba Inayopendekezwa ni wa hasira na usiokuwa na tija kwa maendeleo ya Taifa.

Rais Kikwete alisema: “Waacheni waumini waamue Katiba wanayoitaka wao... hayo matamko niliyoyasoma yamejaa hasira kwa Serikali kupeleka bungeni Muswada wa Mahakama ya Kadhi.”

“Nimeyasoma matamko hayo yote kwa umakini, imenishangaza, imenisikitisha na kunihuzunisha. Siamini kwa nini wamefikia huko kwa kuunga au kutokuunga mkono,” alisema Rais Kikwete. 

Nini maoni yako kuhusu hili swala? Washirikishe wengine habari hii.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
  • * OFFICIAL COMPLAINTS CONCERNING 2015 ELECTIONS FROM LOWASSA
    My fellow citizens! Today on 29 October 2015, through my co-candidate, Hon. Juma Duni Haji have filed…
  • ESTER BULAYA KUTOGOMBEA KUPITIA CCM VITA NI YAKE NA WASSIRA BUNDA MJINI
    Aliyekua Mbunge wa Viti Maalu, Ester Bulaya ametangaza kutokugombea Ubunge kupitia CCM. Jimbo la Bunda…
  • WAZIRI MKUU:CHAMA CHOCHOTE KINAWEZA KUSHIKA DOLA
    Waziri Mkuu Mizengo Pinda UPINZANI KUCHUKUA DOLA Chama chochote cha siasa nchini kina nafasi ya kushika…
  • NAIROBI SENATOR HAS SUED NAIROBI GOVERNOR
    Mike Sonko, Nairobi senator has sued Dr Evans Kidero, Nairobi governor over a defamatory remark he…
  • AJIRA KWA WATANZANIA KATIKA SHIRIKA LA NDEGE LA EMIRATES KWA 2015
    UTANGULIZI Tarehe 22 Januari, 2015 kuanzia saa tano hadi sita mchana, Wizara inatarajia kuongea na…
  • 1 DECEMBER 2015 WORLD AIDS DAY EXHIBITION CANCELLED IN TANZANIA
    President of United Republic of Tanzania Dr. John Magufuli cancelled the climax of HIV and AIDS…
  • SMUGGLER'S IMPOUNDED TANZANITE AUCTIONED IN ARUSHA GEM FAIR
    Arusha. Tanzanite gemstones valued at more than 2.5 billion/- were auctioned during the recently held Arusha…
  • * CABINET RESHUFFLED IN KENYA
    On Tuesday President Uhuru Kenyatta has reshuffled his cabinet replacing Anne Waiguru in the Devolution…
  • $ 92 ML CREDIT FROM INDIA TO IMPROVE WATER ACCESSIBILITY IN ZANZIBAR
    Dar es Salaam, Tanzania. Indian Prime Minister Narendra Modi and Tanzanian …
  •   253 MAJIMBO UKAWA WAMEGAWANA, TABORA MJINI GUMZO NA MENGINE 11
      Majimbo hayo yalitangazwa na wawakilishi wa makatibu wakuu wa UKAWA, John Mnyika (Chadema),…

SOCIALIZE

twitterfacebookgoogle plusemail

IN CASE YOU MISSED IT

FOR INSURANCE SERVICES CLICK HERE