Jeshi la Misri limefanya mashambulizi ya anga dhidi ya vituo vya Dola la Kiislamu nchini Libya, baada ya kundi hilo kusambaza video mtandaoni inayoonyesha Wakristo 21 kutoka Misri wakichinjwa.


Video iliyosambazwa mtandaoni na Dola la Kiislamu inaonyesha Wamisri 21 wakiwa wamevaa nguo za rangi ya chungwa na wakilazimishwa kupiga magoti ufukweni na kisha wakiuliwa mmoja mmoja. Rais wa Misri, Abdel Fatah al-Sisi ameahidi kuongeza nguvu katika kupambana na ugaidi. "Misri ina haki ya kulipiza kisasi kwa wauajia na wahalifu hao ambao hawana utu kabisa. Tutaamua wenyewe namna ya kulipiza kisasi na muda wa kufanya hivyo," amesema al-Sisi.

Jumatatu ndege za kijeshi za Misri zilifanya mashambulizi ya angani katika maficho ya Dola la Kiislamu nchini Libya nayo serikali ya al-Sisi imetangaza siku saba za kuomboleza vifo vya Wakristo hao waliokuwa waumini wa madhehebu ya koptik. Katika tamko lake uongozi wa kanisa la koptik umewataka waumini wake wawe na imani kwamba nchi yao haitatulia hadi pale ambapo waliofanya uasi huu watapewa adhabu wanayostahili.
Mwezi uliopita tawi la Dola la Kiislamu nchini Libya lilikuwa limetangaza kuwa limewateka nyara Wakristo 21 kutoka Misri na inaaminika kwamba hao ndio wanaoonekana kwenye video hiyo.

Tangu kuangushwa kwa utawala wa Muamar Gaddafi mwaka 2011 maelfu ya vibarua wameelekea Libya kutafuta kazi na wengi wao wanatokea Misri. Hata hivyo Wakristo wa koptik mara kwa mara wamelengwa na mashambulizi yaliyofanywa na Waislamu wenye itikadi kali. Rais Abdel Fattah al-Sisi ameahidi kuhakikisha usalama wa wananchi wake walioko Libya. "Nimeiomba serikali iendelee kuwakataza Wamisri kusafiri kwenda Libya wakati huu mgumu ili kuokoa maisha yetu. Nimezitaka pia taasisi husika zichukue hatua kuwawezesha Wamisri warudi nchini mwao," alisema rais huyo.

Bunge la Libya limetoa salamu za rambirambi na kuitaka jumuiya ya kimataifa iiunge mkono Libya katika juhudi za kupambana na wanamgambo. Nao ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini humo umewataka Walibya wote wakatae vitendo vya Dola la Kiislamu. Rais Francois Hollande wa Ufaransa, ambaye alikuwa ameahidi kuiuzia Misri ndege za kijeshi, ameelezea wasiwasi wake juu ya kukua kwa Dola la Kiislamu.


Marekani kwa upande wake imelaani mauaji ya watu hao 21. Msemaji wa ikulu ya White House, Josh Earnest, amesema uovu wa Dola la Kiislamu usiojua mipaka unaiunganisha jumuiya ya kimataifa katika kulipiga kundi hilo.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
  • AKUTWA NA FUNZA ZAIDI YA MIA MOJA 100
    Normal 0 false false false EN-US X-NONE X-NONE …
  • 9 DECEMBER 2015 UHURU DAY CANCELLED - MAGUFULI
    President John Magufuli has ordered the cancellation of 9th December 2015 Independence Day Celebrations for…
  • GOODLUCK JONATHAN TO RECONCILE IN ZANZIBAR POLL STALEMATE
    Zanzibar. The Commonwealth has appointed former President Goodluck Jonathan to lead the charge for the…
  • Tanzania launches Sustainable Energy for All SE4ALL
    Dar es Salaam, Tanzania launches Sustainable Energy for All (SE4ALL) today at Julius Nyerere International…
  • Maandamano ya Kigoma yampa Ujumbe huu Dk.Slaa wa CHADEMA
    Ujumbe wa Dk.Slaa kutoka Kigoma …
  • UFAFANUZI KUHUSU BASTOLA NA RISASI ZA GWAJIMA
    BASTOLA NA RISASI ZA GWAJIMA Tarehe 30/03/2015 waandishi wa habari walifika kituo Kikuu cha Polisi…
  • NAIROBI SENATOR MIKE SONKO AND HIS WEALTH
    Nairobi Senator Mike Sonko In an interview with NTV’s Larry Madowo, Senator Sonko yet…
  • SHERIA YA MAKOSA YA MTANDAO YAANZA RASMI TANZANIA
    Waziri wa Mawasilaiano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa(Mb), akiongea na waandishi wa…
  • Relationship between Arsenal and Manchester City
    Arsenal and Manchester City have had numerous connections over the past 30 years, especially with a…
  • How Cellphone can damage your sexual organs, pregnant women and Children?
    Are you keeping your phone in your pocket? …

SOCIALIZE

twitterfacebookgoogle plusemail

IN CASE YOU MISSED IT

FOR INSURANCE SERVICES CLICK HERE