Mwanaume ambaye amekuwa akitekeleza mauaji ya mateka wa kundi la wapiganaji wa Islamic State ajulikanaye kwa jina la utani "Jihadi John",ametambuliwa.
Bwana huyo ambaye taswira yake akiwachinja mateka kwa kisu bila huruma ndiyo nembo ya wapiganaji hao sasa ametambuliwa kuwa anatokea Uingereza.
Shirika la Habari la BBC limetambua kuwa jina lake kamili ni Mohammed Emwazi.
Emnuazi ameonekana kwenye video kadhaa ya mauwaji ya mateka wa mataifa wa magharibi, akiwemo Mmarekani James Foley, Raia wa Uingereza, Alan Henning na mwaandishi habari wa Japan, Kenji Goto.
 Inaaminika kuwa Emwazi ni raia wa Uingereza na hasa anatokea magharibi mwa London.
Yamkini Emnuazi aliyezaliwa Kuwaiti na mwenye umri wa kati ya miaka 20 -29 alikuwa amefahamika sana na vyombo vya usalama lakini kwa sababu za kiusalama haikuwezekana kumtambua.
Anaaminika amewahi kuishi Somalia mnamo mwaka 2006 na anauhusiano mkubwa na kundi la wapiganaji wa Al Shabab nchini humo.
Polisi nchini Uingereza imeziomba vyombo vya habari kutosambaza habari ambazo hawajazithibitisha kumhusu jamaa huyo kwani uchunguzi unaendelea.
Hata hivyo bado habari za kina kumhusu Jihadi John hazijatolewa.
Mwandishi wa maswala ya Usalama wa BBC Tomi Oladipo anasema kuwa vyombo vya usalama vya serikali za mataifa yanayokaribia Somalia sasa yana kila sababu ya kutahamaki.

Kwa sababu Kuhusika kwake na kundi la Al Shaabab kisha akajiunga na kundi la Islamic State ambalo kwa wakati mmoja lilikuwa linashindana na wanamgambo wa Al Qaeda kuhusu yupi kati yao anayeushawishi
mkubwa
Ishara kuwa Al Shabab inazingatia msimamo mkali wa kidni hata zaidi ya Al Qaeda.
Kwa sababu itakumbukwa kuwa Al Qaeda ilipinga hatua kali ya kuwachinja mateka nchini Iraq na Syria.
Emnuazi ambaye amekuwa akiwabeza mataifa ya Magharibi kabla ya kuwakata shingo naaminika kuwa mtaalamu wa maswala ya kompyuta alisomea chuo kikuu cha Westminster.
Kwa mujibu wa mwandishi wa BBC bwana huyo anaaminika kuwa alikwenda Syria mwaka wa 2012, lakini kabla ya wakati huo majasusi wa Uingereza na Marekani walikuwa hawajajua tishio lake.

Chanzo: http://www.bbc.co.uk/swahili/habari/2015/02/150226_jihadi_john_revealed
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
  • AJIRA KWA WATANZANIA KATIKA SHIRIKA LA NDEGE LA EMIRATES KWA 2015
    UTANGULIZI Tarehe 22 Januari, 2015 kuanzia saa tano hadi sita mchana, Wizara inatarajia kuongea na…
  • MUSWADA WA AJIRA WAPITISHWA BUNGENI, TANZANIA
    Bunge la Tanzania Bunge la Tanzania limepitisha muswada wa sheria ya udhibiti wa ajira za wageni wa mwaka…
  • 13 NEW FACES IN RC RESHUFFLE
    President of Tanzania John Magufuli released the long awaited line-up of regional commissioners (RCs) that…
  • TANZANIA PORTS AND REVENUE AUTHORITY ON INTER-BANK SETTLEMENT SYSTEM
    The Director of National Payment System at BoT, Mr Bernard Dadi, said the Central bank agreed to extend…
  • Today News paper front pages
    Have you read today News paper front page?
  • UFAFANUZI KUHUSU BASTOLA NA RISASI ZA GWAJIMA
    BASTOLA NA RISASI ZA GWAJIMA Tarehe 30/03/2015 waandishi wa habari walifika kituo Kikuu cha Polisi…
  • .MZEE ALIYECHORA NEMBO YA TAIFA AFARIKI DUNIA
    Mzee Francis Maige Kanyasi alipolazwa Hospitali. Dar es Salaam, Muhimbili. Hospitali ya Taifa ya…
  • $ 92 ML CREDIT FROM INDIA TO IMPROVE WATER ACCESSIBILITY IN ZANZIBAR
    Dar es Salaam, Tanzania. Indian Prime Minister Narendra Modi and Tanzanian …
  • 4 U MOVEMENT (TEAM LOWASSA) WAJIUNGA CHADEMA
    Vijana wanao aminika kua ni wafuasi wa Lowassa wahamia CHADEMA.
  • NAIROBI SENATOR HAS SUED NAIROBI GOVERNOR
    Mike Sonko, Nairobi senator has sued Dr Evans Kidero, Nairobi governor over a defamatory remark he…

SOCIALIZE

twitterfacebookgoogle plusemail

IN CASE YOU MISSED IT

FOR INSURANCE SERVICES CLICK HERE