Mwanaume ambaye amekuwa akitekeleza mauaji ya mateka wa kundi la wapiganaji wa Islamic State ajulikanaye kwa jina la utani "Jihadi John",ametambuliwa.
Bwana huyo ambaye taswira yake akiwachinja mateka kwa kisu bila huruma ndiyo nembo ya wapiganaji hao sasa ametambuliwa kuwa anatokea Uingereza.
Shirika la Habari la BBC limetambua kuwa jina lake kamili ni Mohammed Emwazi.
Emnuazi ameonekana kwenye video kadhaa ya mauwaji ya mateka wa mataifa wa magharibi, akiwemo Mmarekani James Foley, Raia wa Uingereza, Alan Henning na mwaandishi habari wa Japan, Kenji Goto.
 Inaaminika kuwa Emwazi ni raia wa Uingereza na hasa anatokea magharibi mwa London.
Yamkini Emnuazi aliyezaliwa Kuwaiti na mwenye umri wa kati ya miaka 20 -29 alikuwa amefahamika sana na vyombo vya usalama lakini kwa sababu za kiusalama haikuwezekana kumtambua.
Anaaminika amewahi kuishi Somalia mnamo mwaka 2006 na anauhusiano mkubwa na kundi la wapiganaji wa Al Shabab nchini humo.
Polisi nchini Uingereza imeziomba vyombo vya habari kutosambaza habari ambazo hawajazithibitisha kumhusu jamaa huyo kwani uchunguzi unaendelea.
Hata hivyo bado habari za kina kumhusu Jihadi John hazijatolewa.
Mwandishi wa maswala ya Usalama wa BBC Tomi Oladipo anasema kuwa vyombo vya usalama vya serikali za mataifa yanayokaribia Somalia sasa yana kila sababu ya kutahamaki.

Kwa sababu Kuhusika kwake na kundi la Al Shaabab kisha akajiunga na kundi la Islamic State ambalo kwa wakati mmoja lilikuwa linashindana na wanamgambo wa Al Qaeda kuhusu yupi kati yao anayeushawishi
mkubwa
Ishara kuwa Al Shabab inazingatia msimamo mkali wa kidni hata zaidi ya Al Qaeda.
Kwa sababu itakumbukwa kuwa Al Qaeda ilipinga hatua kali ya kuwachinja mateka nchini Iraq na Syria.
Emnuazi ambaye amekuwa akiwabeza mataifa ya Magharibi kabla ya kuwakata shingo naaminika kuwa mtaalamu wa maswala ya kompyuta alisomea chuo kikuu cha Westminster.
Kwa mujibu wa mwandishi wa BBC bwana huyo anaaminika kuwa alikwenda Syria mwaka wa 2012, lakini kabla ya wakati huo majasusi wa Uingereza na Marekani walikuwa hawajajua tishio lake.

Chanzo: http://www.bbc.co.uk/swahili/habari/2015/02/150226_jihadi_john_revealed
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
  • How to save your Eyesight from Screens (Computer, Cellphone, Laptop and Television) ?
    Screen is everywhere (Computer, Cellphone, Laptop and TV) Right now you are staring at a screen, ah ah a!…
  • IS MCHINJAJI
    Mwanaume ambaye amekuwa akitekeleza mauaji ya mateka wa kundi la wapiganaji wa Islamic State ajulikanaye kwa…
  • 3 MILLIONS CROWDS PROTEST AGAINST BRAZIL'S PRESIDENT
    Widespread Anger against Brazilian President Dilma Rousseff is mounting as hundreds of thousands of people…
  • CAG REPORT FAULTS NEMC OVER MINING INSPECTIONS
    Professor Mussa Assad NATIONAL Environmental Management Council (NEMC) has failed in its objectives to…
  • NAFASI ZA KAZI BENKI KUU YA TANZANIA
    EMPLOYMENT OPPORTUNITY AT BANK OF TANZANIA The bank of Tanzania, an equal opportunity employer and…
  • PLANE CARRYING 58 PASSENGERS CRASH
    A Taiwanese passenger aircraft with 58 people on board has crashed into a river outside Taiwan’s capital…
  • 3 DAYS STATE VISIT TO ISRAEL - UHURU
    President Uhuru Kenyatta is seen off by Deputy President William Ruto President Uhuru Kenyatta left for…
  • MAWAZIRI NA VIGOGO WALIOSHINDWA KURA ZA MAONI CCM
    Mathias Chikawe Waziri wa Mambo ya ndani ni miongoni mwa wanachama maarufu wa CCM walioshindwa…
  • MAHAKAMA TANZANIA YAPOKEA MSAADA WENYE THAMANI YA DOLLA 95,000
    Mahakama kuu ya Tanzania imepokea msaada wa mashine 38 za kupiga chapa Kutoka Mahakama ya mauaji ya…
  • 2ND MINERAL SANDS REPORT:LIST OF MANY TO BE INTERROGATED
    Dar es Salaaam. Speaking at the State House yesterday after receiving a report from an eight-member team led…

SOCIALIZE

twitterfacebookgoogle plusemail

IN CASE YOU MISSED IT

FOR INSURANCE SERVICES CLICK HERE