Pambano la masumbwi linalosubiriwa na ulimwengu mzima kati ya mabondia wawili bora katika miaka ya hivi karibuni Floyd Mayweather na Manny Pacquiao linakaribia kutokea baada ya uthibitisho wa mazungumzo ya pande mbili zinazowakilisha mabondia hao. Wakala wa Bondia Mfilipino Pacquiao, Fred Sternburg amethibitisha kuwa mazungumzo baina ya kambi za mabondia hawa wawili yanaendelea vizuri na huenda makubaliano yakafikiwa siku sio nyingi. Wakala huyo hata hivyo amekanusha kuwepo kwa uthibitisho wa tarehe ya mabondia hao kupanda ulingoni baada ya kuwepo kwa tetesi kuwa wawili hao watapambana Mei mbili mwaka huu. Pambano hili limewahi kuandaliwa kwa muda mrefu bila mafanikio baada ya mabondia hawa kuonekana wakikwepana hususan Floyd ambaye alikuwa akitoa visingizio vya kila aina ikiwemo kutaka mpinzani wake apimwe vipimo vya dawa za kulevya. Taarifa zaidi zinasema kuwa mabondia hawa wamekubaliana kugawana asilimia 60 kwa 40 ya mapato ya pambano hili ambapo Floyd atachukua asilimia 60 na Manny atachukua asilimia 40.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
  • HAKI ZAKO UWAPO MIKONONI MWA POLISI.
    UWAPO MIKONONI MWA POLISI FANYA HAYA   1. Askari akikuweka chini ya ulinzi muulize…
  • SOUTH SUDANESE PROMISES IGAD TO SIGN PEACE DEAL
    The South Sudanese government decided to sign the IGAD peace deal during a Mini-Summit in Juba. The office…
  • MAGAZETI YA LEO
    Kama kawaida Habari Duniani inakupa vichwa vya habari vya magazeti yote ya kila siku. Leo pia…
  • Nick Cannon files a Divorce from Mariah Carey
    Let's hope Mariah Carey has mastered the art of letting go. According to a new report…
  • MAGAZETI YA LEO TANZANIA
    Habari Duniani inakupa vichwa vya habari vya magazeti. Leo pia kuna habari mpya kwenye magazeti…
  • Amazing Vehicles manufactured in Tanzania, East Afrika - Nyumbu
    Nyumbu A number of African countries chose  institutions of higher learning like universities to…
  • WHO ARE WOMEN ELECTED MP'S IN TANZANIA 2015 ELECTION?
    Following the final result that provided a climax to several days of announcement of results for the…
  • SOMA MAGAZETI YA LEO
    Tanzania Newspaper front pages. Kama kawaida Habari Duniani inakupa vichwa vya habari vya…
  • LOCAL INSURANCE FIRMS CHALLENGED
    Wilson Ndesanjo (Left) and Jean Razafimandimbly (Right) The insurance landscape is bound to change, with…
  • * WABUNGE WAPYA WA UKAWA (CUF, CHADEMA, NLD NA NCCR-MAGEUZI)
    MAJIMBO MAPYA YA UKAWA (CUF, CHADEMA, NLD NA NCCR-MAGEUZI) James Mbatia ashinda Ubunge…

SOCIALIZE

twitterfacebookgoogle plusemail

IN CASE YOU MISSED IT

FOR INSURANCE SERVICES CLICK HERE