KINGUNGE
Kingunge Ngombale Mwiru ‘ametoroka’ chama hicho kutokana na kile alichokieleza kimepoteza mwelekeo.

KINGUNGE AJITOA CCM

Akizungumza na waandishi wa habari nyumbani kwake jijini Dar es Salaam Kingunge amesema, hatojiunga na chama chochote cha siasa “lakini kuanzia sasa mimi sio mwanachama wa CCM,” amesema.

Katika mazungumzo yake na waandishi wa habari, neno ‘mabadiliko’ lilitawala kinywa chake huku akionya kuwa, nguvu ya kupinga mabadiliko ni kubwa.
“Nguvu ya kupinga mabadiliko ni kubwa sana lakini kwa utafiti wangu mimi mzee ni kuwa, nguvu ya kuleta mabadiliko ni kubwa zaidi. Watu wajiamini zaidi na wasubiri tarehe 25 Oktoba mwaka huu,” amesema.

Akielezea namna CCM ilivyopoteza mwelekeo Kingunge amesema chama hicho kimelewa madaraka kutokana na kutawala kwa muda mrefu na kuongeza kuwa ‘wananchi sasa wanataka mabadiliko.”

“Kuongoza nchi ni kama kupanda mlima, utafika mahala pumzi zinakwisha na huwezi kuendelea mbele na ukijaribu kwenda mbele unabaki pale pale, na hivi ndivyo CCM ambapo kimeishiwa pumzi na kimebaki pale pale hakiwezi tena kupanda mlima,” amesema Kingunge.
“Nilipigana nikiwa ndani ya CCM kuangalia nani anafaa ili kuileta nchi kwenye mstari. Niliangalia ili kujua ndani ya chama nani tukimpata anaweza kuipeleka nchi mbio.

“Nilimwona Edward Lowassa kuwa ana sifa kuliko wengi waliojitokeza. Kiongozi lazima akubalike na watu, hii ni sifa tangu wakati wa TANU,”amesema Kingunge na kuongeza;
“Lowassa anakubalika ndani ya CCM na nje ya CCM, ni hivyo pamoja na kutangaziwa mambo ya ajabu kwa miaka minane mfululizo.”
Amesema “kauli zinazotoka sasa hivi, wapinzani hawawezi kushinda. Nyinyi mnajuaje kama hawawezi kushinda? Ukiritimba wa chama kimoja kwa karne moja umetosha, madaraka hulevya.”

Akizungumiza chama tawala kuacha utamaduni wake Kingunge amesema chama hicho kimeacha ‘itikio’ lake lililoasisiwa tangu kuanzishwa kwa chama hicho.
“Wamebadilisha kauli mbiu ya chama badala ya kidumu Chama Cha Mapinduzi – kidumu, sasa wanaitikia kidumu chama tawala,” anasema na kuongeza; “niliwaambia NEC kwamba ukisema hivyo maana yake wewe unataka kubaki kwenye utawala.”

Kingunge amzungumzia Magufuli

Akimzungumzia mgombea urasi wa CCM, Dk. John Magufuli, Kingunge amesema nafasi hiyo ameipata kutokana na chama hicho kuvunja katiba ya chama.
Hata hivyo ameeleza kuwa, tatizo kubwa la wananchi ni uchumi na ajira, “umasikini uanondolewa na uchumi bora,” amesema.

Amesema, Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa aliacha uchumi ukikua kwa asilimia saba na kuingiza nchi kwenye orodha ya nchini zinazokwenda mbio kiuchumi.
“Tazama, Kikwete (Rais Jakaya Kikwete) kapokea uchumi ukikuwa kwa silimia saba na sasa ni miaka 10 uchumi unakuwa karibu na asilimia saba -miaka 10 hii yote tumepiga make time na kiukweli tumerudi nyuma. Mabadiliko ni muhimu ili upate watu wengine wenye pumzi mpya,” amesema.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

SOCIALIZE

twitterfacebookgoogle plusemail

IN CASE YOU MISSED IT

FOR INSURANCE SERVICES CLICK HERE