Waziri wa Mawasilaiano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa(Mb), akiongea na waandishi wa habari. Kushoto ni Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bwana John Mngodo.
Sheria ya Makosa Mtandao, 2015 ambayo ilitangazwa kwenye gazeti la Serikali la Tarehe 14/08/2015 na kupewa Na.328. Pia Sheria ya Miamala ya Kielektroniki, 2015 ambayo ilitangazwa kwenye Gazeti la Serikali la tarehe hiyo hiyo na kupewa Na.329.

Tamko la kuanza utekelezaji rasmi wa sheria hizo mbili yaani ya makosa ya mtandao ya mwaka 2015  na sheria ya miamala ya kielektroniki ya mwaka 2015  lilitolewa na Wizara ya Mawasilaiano, Sayansi na Teknolojia kupitia waziri wake, Profesa Makame Mbarawa. Sheria hizo zinaanza kutumika rasmi kuanzia Jumanne yaani Septemba mosi mwaka huu.

Profesa Makame Mbarawa, Serikali baada ya kujiridhisha kua maandalizi yote muhimu ikiwemo elimu kwa umma na kujenga uelewa kwa watekelezaji wa sheria hizi yamefanyika. Sasa, Sheria hizi zitaanza kutumika rasmi tarehe 01/09/2015.

Kwa hivyo, natoa rain a wito kwa wananchi wote kua tuzingatie “Matumizi Salama na Sahihi ya Huduma za Mawasiliano na Mtandao kwa manufaa ya kila mmoja na kwa maendeleo ya Taifa letu. Mitandao ikitumiwa vema ina faida kubwa sana katika jamii yetu.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

SOCIALIZE

twitterfacebookgoogle plusemail

IN CASE YOU MISSED IT

FOR INSURANCE SERVICES CLICK HERE