Jamhuri ya Muungano wa Tanzania dhidi ya:

Basili Mramba

Daniel Yona

Gray Mgonja

Mahakama ya hakimu mkazi kisutu leo imewahukumu kwenda jela miaka mitatu na faini ya shilingi milioni tano kila mmoja aliyekuwa Waziri wa fedha Basili Mramba na aliyekuwa Waziri wa nishati na Madini Daniel Yona na kumuachia huru aliyekuwa Katibu mkuu Wizara ya Fedha Gray Mgonja.

Washtakiwa hao walikuwa wakituhumiwa kwa pamoja kuisababishia serikali hasara ya shilingi bilioni 11.7 kwa kuisamehe Kodi Kampuni ya Alex Stewart ya Uingereza.
Akisoma hukumu hiyo iliyochukua muda mfupi kwa niaba ya jopo la mahakimu watatu, hakimu Sam Rumanyika amesema washtakiwa hao wametiwa hatiani pasipo shaka dhidi ya ushahidi wa kuthibitisha makosa yao kutoka upande wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo katika shitaka la kumi na moja la kusababisha hasara wamepewa adhabu hiyo ya shilingi milioni tano.

Hata hivyo baada ya hukumu hiyo mawakili wa utetezi wamedai kukata rufaa mahakama kuu baada ya kupata nakala ya hukumu.
Shauri hilo limedumu kwa takribani miaka saba tangu wafikishwe mahakamni hapo mwaka 2008.


Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
  • $ 1 BILLION -VE BALANCE ZIMBABWE HAS WITH WORLD BANK
    Zimbabwe’s bond notes might have eased some of the country’s liquidity challenges, but the World Bank warned…
  • HAVE YOU READ TODAY UK FRONT PAGES NEWSPAPER? READ NOW
    HabaruDuniani brings to you UK front pages Newspaper at your finger tips. Please do not forget to like our…
  • MAYWEATHER ATUA DAR ES SALAAM
    Floyd Mayweather Bondia maarufu duniani kwa sasa Floyd Mayweather baada ya kumpiga Emmanuel "Manny"…
  • 9 DECEMBER 2015 UHURU DAY CANCELLED - MAGUFULI
    President John Magufuli has ordered the cancellation of 9th December 2015 Independence Day Celebrations for…
  • 2015 ACSEE EXAMINATION RESULTS
    Matokeo ya Kidato cha Sita yametangazwa rasmi na Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA). MATOKEO YA KIDATO…
  • First vehicles manufactured in Uganda and Kenya - Kiira and Mobius
    This is a car developed in Uganda by Kiira Motors Corporation (KMC), origionally…
  • MAYWEATHER ATUA DAR ES SALAAM
    Floyd Mayweather Bondia maarufu duniani kwa sasa Floyd Mayweather baada ya kumpiga Emmanuel "Manny"…
  • 36 SPECIAL SEATS MP'S FOR CHADEMA, 10 FOR CUF AND 64 FOR CCM
    October 25, 2015 Tanzania voted for General Elections which resulted to increase in number of special seats…
  • ACACIA TAX FEUD: EXECUTIVE CHAIRMAN MET WITH TANZANIA PRESIDENT
    Tanzania’s President met with Barrick Gold Corp. Executive Chairman John Thornton in an effort to…
  • * ZEC YAFUTA MATOKEO YA UCHAGUZI ZANZIBAR
    Zanzibar: Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi wa Zanzibar – ZEC kwa mamlaka ya Kikatiba aliyopewa,…

SOCIALIZE

twitterfacebookgoogle plusemail

IN CASE YOU MISSED IT

FOR INSURANCE SERVICES CLICK HERE