Joseph Butiku,Mkurugenzi wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere
Joseph Butiku,Mkurugenzi wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere
Joseph Butiku,Mkurugenzi wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere amesema nchi inaongozwa na Katiba, lakini inashangaza viongozi wa chama chake cha CCM na vingine ndiyo wanaongoza kwa kuvunja sheria na taratibu.

“Huko nyuma kulikuwa na matatizo, lakini sasa chama changu (CCM) na vyama vingine ndiyo magwiji wa kuvunja taratibu,” alisema Butiku wakati akichangia hoja jana kwenye mdahalo wa umuhimu wa Kulinda Amani na Umoja uliorushwa moja kwa moja na ITV.

“Mtandao huo iliamua kufanya kazi nje ya CCM kwa sababu itikadi zao na sisi zilitofautiana. Eti wanasema CCM ni chama cha mizengwe kinawachelewesha kutajirika. Sasa hao watu ndiyo wameendelea kuwapo na kusababisha haya matatizo yaendelee,” alisema Butiku.

“Kama baadhi wa watu muhimu wapo nje, sasa mwenyekiti wetu (Rais Jakaya Kikwete) amekwenda kufanya nini huko? Kama viongozi wa CCM wameshampata mtu wanayemtaka (kugombea urais) wanakwenda Dodoma kufanya nini. Huku si kumkejeli Rais Kikwete?” alihoji.

Alisema viongozi hawafuati utaratibu, kila kitu lazima hela. “Sasa tunatoka kwenye utaratibu wetu wa vyama tunashiriki katika kufanya uovu. Kama haki inauzwa, hatuwezi kupata amani. Viongozi wanatoa rushwa hata kabla ya kupewa nchi. Je, wakipewa nchi itakuwaje?” alihoji.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

SOCIALIZE

twitterfacebookgoogle plusemail

IN CASE YOU MISSED IT

FOR INSURANCE SERVICES CLICK HERE