James Lembeli

James Lembeli, Mbunge wa Kahama aliyemaliza muda wake amekataa kubadili msimamo wake wa kutogombea ubunge kupitia CCM akisema atagombea nafasi hiyo kupitia chama kingine.

Akizungumza mjini hapa jana, Lembeli alisema hawezi kubadili msimamo wake wa kuondoka CCM, kutokana na masharti mazito ya kimila aliyopewa kabla ya kutangaza kuondoka katika chama hicho.

Baada ya uamuzi wake, watu mbalimbali, wakiwamo maofisa wa Serikali na wafanyabiashara waliahidi kumsaidia hata nguvu ya kifedha, wakimtaka atengue uamuzi wake achukue fomu katika Jimbo la Kahama Mjini.
Alisema hawezi kukiuka masharti ya kimila kwa kuwa yeye ni mtoto wa chifu. Mtoto huyo wa Chifu Daud Lembeli alisema kabla ya kutoa uamuzi huo alikaa na mama yake mzazi, Maria Kalembo kuanzia saa 10 jioni hadi saa nane usiku akizungumzia suala hilo hadi walipokubaliana.

Alisema baada ya mama yake kukubali na kutoa baraka za kuhama CCM, alipigiwa ngoma za kimila za Waswezi, ambazo hutumika kutoa baraka katika imani za kichifu akisema ndizo zilizohitimisha fursa za kugombea kwake ubunge kupitia chama hicho.
“Najisikia amani kubwa kuondoka CCM, kabla sijachukua uamuzi huu nilikuwa nikiishi kwa presha, hivi sasa nipo huru, niacheni tu kama ni ubunge sikuzaliwa nao na unaweza kuishi bila ubunge na maisha yakawa mazuri,” alisema Lembeli.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
  • 110 MAJINA YA WABUNGE WANAWAKE WA VITI MAALUM
    MAJINA YA WABUNGE WA VITI MAALUM UGAWAJI WA VITI MAALUM KWA KILA CHAMA CHA SIASA UNAZINGATIA IBARA YA 7891)…
  • Maandamano ya Kigoma yampa Ujumbe huu Dk.Slaa wa CHADEMA
    Ujumbe wa Dk.Slaa kutoka Kigoma …
  •   253 MAJIMBO UKAWA WAMEGAWANA, TABORA MJINI GUMZO NA MENGINE 11
      Majimbo hayo yalitangazwa na wawakilishi wa makatibu wakuu wa UKAWA, John Mnyika (Chadema),…
  • * DR.DENIS MUKWEGE NAMED AMONG 100 MOST INFLUENTIAL PEOPLE IN THE WORLD
    The 61-year-old doctor founded the Panzi Hospital in the eastern Democratic Republic of Congo in 1999 to…
  • 1 DECEMBER 2015 WORLD AIDS DAY EXHIBITION CANCELLED IN TANZANIA
    President of United Republic of Tanzania Dr. John Magufuli cancelled the climax of HIV and AIDS…
  • MUTHAURA APPOINTED AS KENYA'S CAPITAL MARKETS AUTHORITY CHIEF EXECUTIVE
    Kenya. Paul Muthaura has been appointed the Kenya's Capital Markets Authority (CMA) chief executive, nearly…
  • WATU MAARUFU WALIO BET KWA MAYWEATHER KUSHINDA
    P DIDDY Floyd Mayweather ndie mtu aliyepata pesa nyingi baada ya pambano akifuatiwa na Manny Pacquiao,…
  • TRAIN COLLIDES WITH TRUCK IN GERMANY
    The accident occurred in Feihung, a German town of about 2,500 people near the border with the Czech…
  • MUHAMMAD ALI IS TEAM PACQUIAO
    Pacquiao and Muhammad Ali "My dad is Team Pacquiao all the way!" Everybody and their dog has…
  • Xavi persuading signing of Santi Cazorla and Silva to Barcelona
    Xavi has hailed the talents of David Silva and Santi Cazorla, admitting he would love to…

SOCIALIZE

twitterfacebookgoogle plusemail

IN CASE YOU MISSED IT

FOR INSURANCE SERVICES CLICK HERE