Serikali ya Jordan imesema itachukua hatua kali za kulipiza kisasi kufuatia kundi la IS kutoa video inayoonesha rubani wake aliyetekwa na kundi hilo akichomwa moto hadi kufa. Serikali ya Jordan imesema inajiandaa kumnyonga mwanamke wa Iraq ambaye kundi la IS lilitaka aachiwe huru. Mfalme Abdullah wa Jordan amelaani tukio hilo na kulitaja kuwa ni tukio la kigaidi la uoga.

"Katika wakati huu mgumu, ni wajibu wa wajordan wote kuungana na kuonesha nguvu katika mapambano dhidi ya ugaidi, tukio hili litatupa nguvu zaidi kupambana na ugaidi."

Mfalme Abdullah ambaye yuko ziarani nchini Marekani amekatisha ziara yake kutokana na tukio hilo na kurudi nyumbani. Rais Barack Obama wa Marekani pia alilaani vikali tukio hilo.

"Hili ni moja ya matukio yanayoonesha ukatili na unyama wa kundi hili, nadhani tutaongeza juhudi na nia yetu kwenye ushirikiano wa dunia kuhakikisha kundi hilo linashindwa."


Katibu Mkuu wa Umoja wa mataifa Bw Ban Ki Moon amelaani tukio hilo, na kusema kundi la IS halithamini maisha ya binadamu.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

SOCIALIZE

twitterfacebookgoogle plusemail

IN CASE YOU MISSED IT

FOR INSURANCE SERVICES CLICK HERE